Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 53 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 698 2023-06-22

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -

Je, lini soko la samaki Mbamba Bay litaanza kutumika?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Jimbo la Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa soko la samaki la Mbamba Bay unafanyika kwa awamu ambapo awamu ya kwanza ulianza mwezi Mei 2021 na kukamilka mwezi Machi, 2022. Katika awamu ya kwanza Serikali ilijenga jengo kuu ambalo lina vizimba au meza za kuuzia samaki. Kwa sasa, Serikali inaanza awamu ya pili ya ujenzi wa soko hilo ambao unahusisha ujenzi wa miundombinu ya maji safi, maji taka pamoja na choo. Aidha, zabuni ya ujenzi huo imeshatangazwa na kufunguliwa Tarehe 23 Mei, 2023. Kazi ya uchambuzi na tathmini ya nyaraka za zabuni inaendelea ili kumpata mzabuni wa kuanza kazi hiyo.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali inatambua umuhimu wa soko hilo na litaanza kutumika tu mara tu baada ya ujenzi wa miundombinu hiyo kukamilika.