Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 25 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 218 2022-05-18

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara Jimbo la Serengeti hasa za vijijini ambazo hutumika kusafirishia mazao?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Jimbo la Serengeti, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Serengeti ina jumla ya mtandao wa barabara wenye urefu wa kilometa 971.78 zinazohudumiwa na TARURA. Barabara zenye hali nzuri ni kilometa 131.82, wastani kilometa 194.97 na mbaya ni kilometa 644.99. Katika mwaka wa fedha 2020/2021 barabara zenye urefu wa kilometa 121.24 zilifanyiwa matengenezo ya aina mbalimbali kwa gharama ya shilingi milioni 965.85.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 2.494 kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilometa 152.24 ambazo ujenzi na matengenezo ya kilomita 138.74 za barabara na vivuko 34 yamekamilika. Matengenezo haya yanajumuisha barabara ya Mugumu – Masangula – Kemgesi kilometa 9.0, Kwitete – Mosongo – Wagete kilometa 25, Nyichoka – Maburi kilomita 6.0 na Barabara ya Nyamakobiti – Iselesele kilometa 7.1.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 2.41 kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilomita 72.81 na vivuko vidogo 18.