Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 25 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 219 2022-05-18

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:-

Je, ni lini Mradi wa Climate Change utawafikia wananchi wa Tarafa ya Chamriho wanaokabiliwa na tatizo la ukame?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Bunda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linasimamia utekelezaji wa Mradi uitwao Bunda Climate Resilience and Adaptation Project wenye kiasi cha dola za Kimarekani 1,400,000 unaofadhiliwa na Adaptation Fund. Mradi huo unatekelezwa Wilayani Bunda katika maeneo ya Kata za Kasuguti, Namhura, Iramba, Neruma, Mahyolo, Igundu na Butimba. Kwa mujibu wa andiko lililoidhinishwa, Tarafa ya Chamriho kwa sasa iko nje ya mradi huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Makamu wa Rais itaendelea kutafuta fursa mbalimbali za miradi ya Mazingira kwa kushirikiana na Halmashauri ya Bunda ili kukabiliana na changamoto iliyopo katika Tarafa ya Chamriho.