Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 25 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 220 2022-05-18

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:-

Je, ni lini wananchi wa Wilaya ya Mbeya waliopisha mradi wa njia kuu ya kusafirisha umeme mkubwa wa Kilovolti 400 watalipwa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANESCO inaendelea na maandalizi ya ujenzi wa mradi wa njia ya kusafirisha umeme mkubwa wenye msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa kupitia Mbeya, Tunduma hadi Sumbawanga yenye urefu wa kilomita 616. Mradi huu pia unahusisha ujenzi wa Vituo vya Kupoza Umeme vya Iringa, Kisada, Mbeya, Tunduma na Sumbawanga pamoja na ujenzi wa kilomita nne za njia ya umeme msongo wa kilovoti 400 kwenda kwenye mpaka wa Tanzania na Zambia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uthamini unafanywa na TANESCO kwa kushirikiana na Wathamini wateule wa Wilaya za Iringa, Mufindi, Mafinga, Mbarali, Mbeya, Jiji la Mbeya, Mbozi, Tunduma, Momba na Sumbawanga ambapo katika maeneo hayo mradi unapita. Hadi kufikia Mwezi Aprili, 2022, majedwali ya fidia ya Halmashauri za Iringa, Mufindi, Mafinga, Momba na Mbarali tayari yameshaidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali na kukabidhiwa TANESCO kwa ajili ya kuanza maandalizi ya malipo. Majedwali ya Wilaya za Mbeya, Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Mbozi, Tunduma na Sumbawanga yapo katika hatua za mwisho za ukamilishwaji. Fidia hizi zinatarajia kuanza kulipwa mwaka wa fedha 2022/2023.