Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 26 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 225 2022-05-19

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya Makongolosi – Rungwa – Mkiwa kwa awamu. Taratibu za manunuzi ya mkandarasi wa kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Noranga – Itigi eneo la Mlongoji yenye urefu wa kilometa 25 zipo katika hatua za mwisho za kusaini mkataba. Aidha, Serikali inaendelea na taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa kujenga sehemu ya kilometa 31.9 kati ya Itigi Kitongoji cha Mlongoji na Mgandu kwa kiwango cha lami. Kwa sehemu iliyobaki Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi. Ahsante.