Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 27 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 229 2022-05-20

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za mitaa ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa kwa kiwango cha lami kupitia Miradi ya TACTIC?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Jimbo la Kondoa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuendeleza Mpango wa Kuboresha Miundombinu ya Msingi katika Miji Nchini, Serikali kupitia Mradi wa Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness Project (TACTIC) utakaotekelezwa katika miji 45. Mradi huo utatekelezwa katika Halmashauri za Majiji, Manispaa na Miji kupitia mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia wenye jumla ya Dola za Kimarekani milioni 500, baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa na Benki ya Dunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Mji wa Kondoa ni miongoni mwa miji 45 nchini ambayo imepewa kipaumbele cha kupata ufadhili wa Mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu katika Miji. Aidha, Halmashauri hii ipo kwenye kundi la tatu lenye jumla ya miji 18 ambayo inatarajiwa kuanza kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa miradi iliyopendekezwa na Halmashauri husika katika mwaka wa fedha 2022/2023.