Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 27 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 230 2022-05-20

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha kwa ajili ya kumalizia Miradi ya Afya iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdukarimu Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mchango wa wananchi katika ujenzi wa miundombinu ya kutolea huduma za afya kote nchini. Aidha, Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati nchi nzima katika kila jimbo. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali ilitenga fedha Shilingi bilioni 27.75 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati 555 ambapo jumla ya Shilingi bilioni 26.95 zilitolewa na Serikali kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi bilioni 38.2, zimetengwa kwa ajili ya kukamilisha maboma ya zahanati 763 yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambapo maboma 564 yanakamilishwa kwa fedha ya ruzuku ya Serikali na maboma 199 kwa fedha za halmashauri mapato ya ndani, ambapo jumla ya fedha shilingi bilioni 30.98 zimekwishatolewa mpaka sasa, ikijumuisha shilingi bilioni 26.92 ruzuku ya Serikali na shilingi Bilioni 4.06 mapato ya ndani ya halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga shilingi bilioni 15 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati 300.