Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 27 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 231 2022-05-20

Name

Capt. Abbas Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Fuoni

Primary Question

MHE. ASYA MWADINI MOHAMED K.n.y. MHE. KAPT. ABBAS ALI MWINYI aliuliza:-

Je, ni kero gani za Muungano bado hazijapata ufumbuzi hadi sasa; na ni jitihada gani zinafanyika ili kero zilizosalia zipate ufumbuzi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Kapt. Abbas Ali Hassan, Mbunge wa Fuoni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kero za Muungano ambazo bado hazijapatiwa ufumbuzi mpaka sasa ni saba ikiwa ni pamoja na:

(i) Moja ni mgawanyo wa Mapato yatokanayo na Hisa za SMZ zilizokuwa katika Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki na faida ya Benki Kuu;

(ii) Usajili wa Vyombo vya Moto;

(iii) Ongozeko la gharama za umeme kutoka TANESCO kwenda ZECO;

(iv) Malalamiko ya Wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili;

(v) Kodi ya Mapato (PAYE) na kodi ya Mapato inayozuiliwa (Withholding Tax);

(vi) Mapendekezo ya Tume ya Pamoja ya Fedha;

(vii) Changamoto ya uingizaji wa sukari katika soko la Tanzania Bara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Makamu wa Rais imeendelea kuimarisha uratibu wa utatuzi wa hoja zilizobaki kati ya sekta zenye hoja za pande zote mbili za SMT na SMZ na kuwasilisha maamuzi kwenye Sekretarieti ya Kamati ya Pamoja yenye jukumu la kufuatilia hatua za utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya Pamoja na kutoa ushauri kwa sekta zenye hoja namna ya kuendelea kuzitatua hoja hizo. Aidha, Serikali za pande zote mbili zinashirikiana kwa karibu kuhakikisha vikao vya pamoja vilivyokubaliwa kwa ajili ya kupata ufumbuzi hoja zilizosalia vinaendelea kama utaratibu ulivyopangwa.