Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 27 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 232 2022-05-20

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Ndege katika Mkoa wa Shinyanga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Santiel Eric Kirumba, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga kitajengwa kwa ufadhili wa Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank – EIB).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfadhili wa mradi huu tayari ameshaleta fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi. Aidha, Serikali imekwishafanya marekebisho ya mkataba na kuwasilisha kwa Mfadhili ili atoe idhini (no objection) kwani kutakuwa na mabadiliko ya gharama ikilinganishwa na wakati mkataba huo uliposainiwa mwaka 2017. Kazi za ujenzi wa mradi huu zitaanza mara moja tutakapopata no objection kutoka Benki ya Uwekezaji ya Ulaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.