Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 27 Water and Irrigation Wizara ya Maji 234 2022-05-20

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:-

Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Basotu kwa ajili ya Vijiji zaidi ya tisa (9) utaanza kutekelezwa Wilayani Hanang’?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samwel Xaday Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang’, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa kutuma Ziwa Basotu kwa ajili kupeleka maji katika vijiji kumi vya Diling’ang, Wandela, Gawindu, Bassotu, Muungano, Milingori na Ming’enyi vilivyopo Wilaya ya Hanang. Utekelezaji wa awamu ya kwanza utanufaisha Kijiji cha Bassotu ambapo kazi zinazofanyika ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji, vituo 13 vya kuchotea maji, na ulazaji wa bomba lenye urefu wa kilometa 14. Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Julai, 2022 na utanufaisha wananchi wapatao 16,553.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 utekelezaji wa mradi huu wa maji utaendelea katika vijiji tisa vilivyobaki ili kuimarisha huduma ya upatikanaji wa maji kwa vijiji vyote.