Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 307 2022-06-01

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: -

Je Serikali ina mpango gani wa kuunganisha barabara Kata za Ulaya, Kisanga, Malolo na Uleling’ombe katika Jimbo la Mikumi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deniss Lazaro Londo Mbunge wa Jimbo la Mikumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali inaifanyia matengenezo barabara ya Kidodi – Vidunda yenye urefu wa kilomita 4.14 ambayo itawezesha uunganishaji wa Kata za Vidunda na Kidodi. Pia, ujenzi wa daraja la Ruhembe kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.00 utawezesha kuunganisha Kata za Ruhembe na Kidodi.

Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/2023, TARURA imetenga Shilingi Bilioni 1.00 kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Ulaya – Kisanga kilomita 42.1 ambayo itaunganisha Kata za Ulaya na Kisanga. Aidha, kiasi cha Shilingi Milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya ukamilishaji wa daraja la Ruhembe linalounganisha Kata za Ruhembe na Kidodi.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kuunganisha Kata ya Malolo na Uleling’ombe katika Jimbo la Mikumi kulingana na upatikanaji wa fedha.