Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 396 2022-06-16

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE K.n.y MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa kiasi cha fedha ilizoahidi kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Malula Kibaoni hadi Ngerenanyuki?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni Moja kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Malula - King’ori – Leguluki - Ngarenanyuki yenye urefu wa kilomita 33.7 kwa kiwango cha changarawe. Ujenzi wa Barabara hiyo umefikia asilimia 70 ambapo kazi zilizotekelezwa hadi sasa ni uchongaji wa barabara kilomita 33.7, karavati 16 na uwekaji wa tabaka la changarawe kilomita Tisa umekamilika na ujenzi unaendelea. Ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Tarehe 28 Juni, 2022.