Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 31 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 270 2022-05-26

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO K.n.y. MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itarekebisha Sheria ya Utakatishaji Fedha inayozuia dhamana kwa Watuhumiwa hata kwa makosa ya kawaida?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kifungu cha 12 cha Sheria ya Kudhibiti Utakasishaji wa Fedha Haramu, Ufadhili wa Ugaidi na Ufadhili wa Silaha za Maangamizi, Sura 423, kinabainisha makosa ya utakasishaji wa fedha haramu pekee. Sheria hiyo haihusishi makosa mengine yoyote, hususan kuzuia au kutozuia dhamana kwa watuhumiwa wa makosa ya kawaida. Aidha, utaratibu wa dhamana kwa makosa mbalimbali, ikiwemo utakasishaji wa fedha haramu unasimamiwa na Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura 20.

Mheshimiwa Spika, kwa msingi huo, hakuna sababu ya kurekebisha Sheria ya Kudhibiti Utakasishaji wa Fedha Haramu, Ufadhili wa Ugaidi na Ufadhili wa Silaha za Maangamizi, Sura 423 kwa kuwa haizuii dhamana kwa watuhumiwa wa makosa ya kawaida. Ahsante.