Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 273 2022-05-27

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja katika Mto Loya?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TARURA katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 imetenga shilingi milioni 318.90 kwa ajili ya usanifu wa daraja la Mto Loya ambapo tayari kazi ya usanifu ilianza tarehe 22 Desemba, 2021 na inategemea kukamilika tarehe 21 Juni, 2022 ambapo gharama halisi za ujenzi zitakuwa zimejulikana. Kazi hiyo ya usanifu inafanywa na Mhandisi Mshauri Advanced Engineering Solutions ya Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kujulikana kwa gharama za ujenzi huo ambao unalenga kujenga daraja kubwa na daraja la watembea kwa Miguu ikiwa ni pamoja na kujenga barabara approach road yenye urefu wa kilometa 13, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.