Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 276 2022-05-27

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto ya uhaba wa walimu, madarasa, samani na miundombinu mingine inayochagizwa na utekelezaji wa Sera ya Elimu bila Malipo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuchukua hatua kukabiliana na upungufu wa walimu katika shule za msingi na sekondari nchini kwa kuajiri walimu na kuwapanga katika maeneo yenye uhaba, kufanya msawazo wa walimu katika maeneo yasiyo na walimu wa kutosha

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika kukabiliana na changamoto ya miundombinu ya elimu inaendelea kujenga shule mpya, madarasa yenye samani ndani yake na kuboresha miundombinu chakavu kupitia bajeti ya Serikali na miradi ya kuboresha elimu kama vile BOOST, SEQUIP, EP4R na GPE LANES II.