Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 277 2022-05-27

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakifanyia matengenezo Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni na ujenzi wa nyumba za askari?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya tathmini ya uchakavu wa Kituo cha Polisi Micheweni na kubaini kuwa kiasi cha fedha shilingi 51,000,000 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa kituo hicho. Aidha, ujenzi wa jengo la hanga la kituo hicho umefikia kwenye hatua za kumalizia na kiasi cha fedha shilingi 57,000,000 zinahitajika. Ukarabati wa kituo pamoja na umaliziaji wa ujenzi wa jengo la hanga utafanyika kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.