Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nakushukuru kwa kunipa hii nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa nimeliuliza hili swali mara mbili hapa Bungeni na majibu ya Serikali yamekuwa kwamba Halmashauri bado haijawasilisha andiko; na kwa kuwa tayari Waziri ana taarifa kwamba kuna andiko ambalo limeshaandikwa, lakini limechukua muda mrefu.

Sasa je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba inaweka mkakati wa kuzisaidia Halmashauri zote nchini ambazo zinahitaji kuja na hii miradi ya kimkakati ili ziwasilishe hii miradi kwa wakati?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Waziri yupo tayari kuambatana nami kwenda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni ili akajionee hali halisi ya stendi ya mabasi ambayo ipo? Nashukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dkt. Chaya amekuwa akifuatilia sana sana miradi ya maendeleo kwa wananchi wa Jimbo la Manyoni Mashariki ikiwemo stand hii na ni kweli ameuliza hapa mara pili. Na nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kwamba andiko hili limekuwa likisubiriwa kwa muda mrefu na sasa tunatoa maelekezo kwa tarehe hiyo ambayo wameji-comment tarehe 30 Juni, lazima andiko liwe limefikishwa hapa ili Serikali ifanye tathmini na kuona namna ya kuwaletea wananchi wa Manyoni maendeleo.

Mheshimiwa Spika, niko tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge kwenda Manyoni, tutakubaliana baada ya Bunge hili tuweze kwenda kuona stand hiyo.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 2

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Katika Manisapaa ya Mtwara Mikindani, stand ya mabasi makubwa iliyopo eneo la Chipuputa hali ya miundombinu yake ni mbaya, mvua ikinyesha maji yanajaa wasafiri wanapata shida. Nataka kujua tu kauli ya Serikali, watarekebisha lini ili stand ile iweze kutumika kwa matumizi ambayo yamekusudiwa? Nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tunza Malapo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Tunza kwa kufuatilia maendeleo ya wananchi wa Mtwara, lakini nimhakikishie kwamba tumetoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri zetu kuhakikisha yale maeneo ambayo ni vipaumbele ambayo yanagusa moja kwa moja maslahi ya wananchi zikiwemo stand, kufanya tathmini kuona uwezekano wa kufanya matengenezo kwa kufanya mapato ya ndani au kuandika maandiko maalum.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani kufanya tathmini hiyo au kufanya matengenezo au kuleta maombi kwa ajili ya kufanya kupitia Serikali Kuu. Ahsante.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 3

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mbogwe inazo stand mbili, lakini hali yake ni mbaya sana hasa mvua ikinyesha, mabasi huwa yanapata shida kupita.

Je, ni nini kauli Serikali kuweza kuzikarabati stand hizo ili zikae kwenye standard?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nicodemas Maganga, Mbunge wa Jimbo la Mbogwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Maganga kwa namna anavyowasemea wananchi wa Mbogwe. Lakini nitoe maelekezo kwamba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe afanye tathmini ya gharama zinazohitajika kufanya matengenezo kwenye stand hizi mbili ambazo ni chakavu sana ili tuone kupitia mapatao ya ndani wanaweza kufanya matengenezo, lakini kama mapato ya ndani hayatoshelezi basi waweze kuwasilisha maandiko ya kimkakati Serikali itafute fedha kwa ajili ya kutengeneza stand hizo. Ahsante.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Mji wa Kibara ndiyo makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, lakini kwa bahati mbaya mpaka sasa hivi hatuna stand ya mabasi. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na suala hilo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Kajege kwa kazi nzuri na kubwa anayowafanyia wananchi wa Mwibara, lakini nimuelekeze Mkurugenzi na Halmashauri kwa ujumla kuainisha eneo hili kama ni eneo la kimkakati na kwamba ni mahitaji ya Halmashauri ili kuona uwezekano wa kupata stand katika eneo hilo.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 5

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; kwa kuwa stand nyingi inakuwa unaingia tu kwa kuwa huna la kufanya lakini hazina mwelekeo wa stand; kwa nini Serikali haiji na model stand kwa Makao Makuu ya Mikoa zikafanana zote kama vile ilivyo vituo vya polisi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asha Juma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze kwa kazi kubwa anayoifanya kuwasemea Watanzania kwa ujumla wake, lakini Serikali tulishatoa maelekezo na standard drawings za stand za ngazi ya Halmashauri, Mikoa lakini na majengo mengine. Kwa hiyo suala hili tunaendelea kuliboresha, kumekuwa na utofauti, kati ya mikoa na mikoa, lakini tumeshatoa sasa utaratibu ambayo ile michoro yote itakuwa inafanana. Ahsante.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 6

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuwa usafirishaji wa abiria ni jambo la muhimu kwenye nchi yoyote yenye ustaarabu.

Je, Serikali haioni ni muda sahihi sasa wa kuhakikisha wanatengeneza mkakati maalum wa kuzijenga stand kwenye miji inayoendelea ikiwemo Mlandizi ili kuachana na mipango ya mradi wa kimkakati ya Halmashauri isiyotekelezeka?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mwakamo kwa ambavyo anawakilisha ipasavyo wananchi wa Jimbo la Kibaha Vijijini, lakini Serikali ilishaweka mkakati tayari wa kujenga stand katika maeneo yote ambayo yanahitajika na ndiyo maana tunatekeleza kwa njia ya aina mbili; moja kwa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa gharama zile ambazo zinafikika lakini kwa kutumia miradi ya kimkakati.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mkakati tayari upo na tunaendelea kuutekeleza, suala ni Halmashauri pia kuhakikisha kwamba wanawasilisha mahitaji hayo Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji.

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 7

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Spika, ahsante, stand ya Lindi Manispaa bado haiko vizuri, mabasi yote yanayotoka Mtwara, Songea na mkoa mzima kwa ujumla yanapitia pale.

Je, Serikali ina mkakati gani kujenga stand ile kuu? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tecla Ungele, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Ungele amekuwa ni miongoni mwa Waheshimiwa Wabunge ambao wanawasemea sana wananchi kwa Watanzania kwa ujumla na wananchi wa Mkoa Lindi, naifahamu sana stand ya Manispaa ya Lindi kwa sababu nimekuwa kule kwa miaka kadhaa, ninafahamu kwamba tunahitaji kuijenga, tuotoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, kutambua hii ni kipaumbele cha Halmashauri kufanya tathamini ya gharama na kuona kama inaweza ikajengwa kwa mapato ya ndani au wawasilishe kama mradi wa kimkakati. Ahsante.