Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji Kata ya Iwawa Makete Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwanza niipongeze Serikali kwa sababu mradi huu unatumia takribani shilingi 3,000,000,000 kwenye utekelezaji wake lakini tayari wameshatoa shilingi 500,000,000. Ni lini Serikali itatoa shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya kukamilisha mradi huu kwa ajili ya wananchi wa Kata ya Iwawa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuna mradi wa Matamba - Kinyika ambao Serikali imetumia zaidi ya shilingi bilioni 2.8 kuujenga, lakini hadi leo hamjaukamilisha takribani miaka saba.

Ni lini Serikali itakabidhi mradi huu kwa wananchi wa Kijiji cha Nungu, Ng’onde, Mbela na Hitani ili waweze kupata huduma ya maji kwa sababu imebaki tu eneo la distribution kwa maana ya usambasaji? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Festo Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi ambao tayari tumeshautolea shilingi milioni 500 na utekelezaji wake unakwenda vizuri ni ule mradi ambao umetumia fedha za mapambano dhidi ya UVIKO-19 na fedha iliyobaki tutaendelea kutoa kuanzia mwezi huu wa Juni, tutaendelea kuongeza fedha. Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa tuonane tuliweke sawa hili kwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Mradi wa Matamba - Kinyika ni kweli mradi umechukua muda mrefu, lakini ni katika ile miradi ambayo ilikuwa ni chechefu na tayari tunaendelea kuikwamua, hivyo mradi huu pia kwa sasa hivi umeshafikiwa hatua nzuri ni zaidi ya asilimia 80 umeshaweza kutekelezwa, tutakuja kuumalizia hivi punde na watu wa IRUWASA watakabidhi kwa watu wa NKOMBEWASA ili waweze kufanyakazi ndani ya mkoa wao.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji Kata ya Iwawa Makete Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mradi wa Maji wa Uhambi Ngeto ambao umetengewa fedha kwa mwaka huu umekuwa ukitafutiwa mkandarasi tangu mwaka umeanza na mpaka sasa mkandarasi hajaanza kazi.

Je, ni lini mkandarasi huyu atapata mkataba ili aweze kufanyakazi kukamilisha mradi ule?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu swali la Mheshimiwa Justin, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli mradi huu bado haujapatiwa mkandarasi lakini taratibu zipo mwishoni kabisa. Mheshimiwa Mbunge naomba tuwasiliane baada ya hapa tuliweke sawa suala hili.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji Kata ya Iwawa Makete Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, tunaishukuru sana Serikali kwa mradi mkubwa wa maji wa Kibamba, Kisarawe na Pugu ambao tayari umeaanza kusambazwa kwenye kata mbalimbali za Jimbo la Ukonga. Swali langu je, Serikali sasa ina mpango gani wa usambazaji wa Kata ya Kitunda, Mzinga, Kivule na Kipunguni ambazo hazina usambazaji wa maji haya safi na salama ya DAWASA? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyokiri Serikali tumeendelea kufanya kazi nzuri kwa Mkoa wa Dar es Salaam na katika maeneo haya aliyoyataja tayari tunafedha zaidi ya shilingi bilioni 25 kwa ajili ya mradi huu na sasa hivi tayari mkandarasi ameshapatikana tunaratajia kufika mwishoni mwa mwaka 2022 haya maeneo yote usambazaji wa maji utakuwa umewafikia.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji Kata ya Iwawa Makete Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniruhusu kuuliza swali la nyongeza.

Tunayo miradi ya World Bank ambayo ilianzishwa katika Jimbo langu la Nanyumbu, miradi ile ni chechefu; je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba miradi ili chechefu inafanyakazi katika Kata ya Mnanje, Kijiji cha Holola, Kata ya Nandete, Chiwilikiti na Ulanga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tuna speed kubwa sana ya kuhakikisha miradi yote iliyokaa muda mrefu inakamilika. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais ameendelea kutupatia fedha na tunaona namna kazi kubwa anayoifanya Mheshimiwa Rais kwa kuijali Wizara ya Maji na kuona kwamba akina mama wanatua ndoo kichwani.

Mheshimiwa Mbunge kwenye maeneo haya uliyoyataja tunakuja kuyafanyia kazi. (Makofi)