Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza michango kwa Wanafunzi wanaojiunga Kidato cha Kwanza?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na ninamshukuru Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza:

Mheshimiwa Spika, kwanza; kwa kuwa sasa tuna elimu bure ya sekondari na mpaka Kidato cha Sita. Ninashukuru kwa hilo kwa Serikali, nimshukuru Mama Samia kwa kutoa elimu bure kwa Kidato cha Tano na cha Sita. Sasa lipi Serikali itafanya kusamehe michango ya sekondari 20,000? Kusamehe michango ya Kidato cha Sita na cha Tano ya 70,000 au kutoa michango ya sekondari ambayo inafikia Shilingi Laki Tano au michango ya Kidato cha Sita ambayo inafikia Shilingi Milioni Moja, kipi kifanyike sasa? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa swali lake lilikuwa ni la jumla na nimwambie tu kwamba baada ya elimu bila ada maana yake wanafunzi wale hawalipi ile ada ambayo walikuwa wanalipa ya Shilingi 20,000 kwa Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne. Maana yake na hivi tunavyokwenda kwa Kidato cha Tano na Kidato cha Sita ambapo ada kwa miaka yote imekuwa ni Shilingi 70,000 maana yake sasa hivi wazazi hawatalipa hiyo ada ya Shilingi 70,000. Kwa hiyo, huo ndiyo msimamo wa Serikali kuhakikisha kwamba tunawasaidia wananchi wote wa Tanzania ili waweze kupata elimu bila malipo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu hiyo michango mingine tunaendelea kuiangalia ili kuhakikisha kwamba haiathiri masomo ya wanafunzi na wazazi kuhakikisha watoto hawa wanapata elimu bora. Ahsante sana.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza michango kwa Wanafunzi wanaojiunga Kidato cha Kwanza?

Supplementary Question 2

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Kumekuwa na michango mingi sana hasa kwa hawa wanafunzi wanaojiunga na Kidato cha Tano. Nina mwanafunzi ambaye hana wazazi hana familia, alikuwa anaenda Bwiru Sekondari, nimelazimika kutoa fedha nyingi mara nne zaidi ya ile fedha ya ada.

Nini sasa tamko la Serikali leo juu ya shule hizo ambazo michango ni mikubwa mara Nne zaidi ya fedha ambazo unatozwa za ada?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monnie Mbunge wa Jimbo la Chemba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kwamba yote lazima iwe imepitishwa kwa kuzingatia mazingira yaliyopo. Kama kuna shule ama kuna eneo lolote lina michango mikubwa tunaomba taarifa hizo ofisi ya Rais TAMISEMI ili tuweze kuchukua hatua katika hayo maeneo ambayo wamezidisha michango.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, michango ambayo imezidi kiwango ni michango ambayo haikubaliki na Serikali tulishatoa kauli yetu.(Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza michango kwa Wanafunzi wanaojiunga Kidato cha Kwanza?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri kumekuwa na lugha ya pre-form one ambayo inatumika sana kwenye shule binafsi na ina michango mingi sana kwa wazazi wanaopeleka watoto kwa masomo hayo. Mnatoa tamko gani kama Serikali kuondoa hili neno la pre-form one kwa sababu inaongeza gharama kwa familia na wazazi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, masuala yote yanayohusu shule binafsi yanashughuliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, nasi kama wadau tunatambua mchango mzuri ambao unatolewa na shule binafsi katika kukuza elimu bora nchini. Kwa hiyo, nimuelekeze Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tumelipokea na tutalifikisha Wizara ya Elimu ili waweze kuchukua hatua ambazo zinastahili.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza michango kwa Wanafunzi wanaojiunga Kidato cha Kwanza?

Supplementary Question 4

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na Serikali kutoa elimu bure kwa wanafunzi wetu lakini bado kuna michango mingi sana ambayo inakera kwa wazazi. Mfano katika shule za kwetu huko vijijini, shule inaambiwa iwe ya bweni, mzazi anahitajika atoe mpaka kitanda, na kuna baadhi mpaka hela ya chakula. Sasa inapotokea mzazi ameshindwa kutoa hizo huduma ambazo anatakiwa achangie mtoto anaadhibiwa.

Je, Serikali ina kauli gani kuhusu hizi shule ambazo zinatoa adhabu kwa wanafunzi, badala ya kwa mzazi ambaye ameshindwa kuhudumia hiyo michango?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake fasaha.

Mheshimiwa Spika, pia niipongeze sana Young Africans kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pamoja na sera ya elimu bila malipo, ambayo Serikali tunaendelea kuitekeleza, katika hili nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuendeleza sera ya elimu bila malipo na kama Mheshimiwa Waziri wa Fedha alivyosoma hoja yake ya Bajeti Kuu, na sasa hivi tunaenda mpaka Form Five na Form Six tunamshukuru na kumpongeza sana Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Spika, kwenye upande wa michango ya wazazi, kwenye masuala ya uendeshaji wa shule za sekondari, upo mwongozo ambapo Bodi au Kamati za Shule zinashirikisha wazazi au walezi. Kwa hiyo, ningependa kutoa maelekezo kwa Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu kushirikisha wazazi au walezi kupitia mwongozo ambao Serikali imeutoa namna tunavyoshikirikisha wazazi au walezi kwenye ile michango tunahitaji kushirikisha wazazi au walezi kuendesha shule zetu.

Mheshimiwa Spika, mwongozo upo bayana kwa hivyo maelekezo yangu kwa Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu, ni kuwashirikisha wazazi kupitia vikao ambavyo vimepangwa kwa taratibu zilizopo, bodi za Shule na Kamati za Shule, hayo ndiyo maelekezo yangu. Ninashukuru. (Makofi)

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza michango kwa Wanafunzi wanaojiunga Kidato cha Kwanza?

Supplementary Question 5

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kutokana na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini kwa kuwa Wabunge wote katika swali hili linaonesha ni namna gani wananchi wanakerwa pamoja na kuwa na huo mwongozo.

Je, Serikali haioni ipo haja sasa ya kuwaelekeza Walimu na hizo Bodi wasitumie mwongozo huo kama uchochoro wa kuwapatia wazazi mzigo mzito?(Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumepokea wazo la Mheshimiwa Mbunge na tunatoa maelekezo kuwakumbusha shule zote nchini juu ya utekelezaji wa mwongozo huo. Ahsante sana.