Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, Serikali ina mikakati gani ya kutujengea mahakama ya Mwanzo katika Tarafa ya Manyovu na Muyama?

Pili, kwa kuwa Tarafa ya Manyovu ina Kata 14 ambazo kijiografia zimesambaa umbali mrefu, Kata Saba zina umbali kwenda Makao Makuu ya Tarafa kati ya kilometa 50 – 84. Je, Serikali inaweza kutusaidia Mahakama mbili za mwanzo katika Tarafa moja ya Manyovu? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kuhusu ujenzi wa Mahakama hizi mbili alizoziomba katika Tarafa ya Manyovu na Muyama hizi zipo katika mpango ambao tulikwishaueleza huko nyuma kwamba tunakwenda kujenga Mahakama katika Tarafa zote nchini na program hii itakwisha 2025 ambapo tuna uhakika Tarafa zote zitakuwa zimepata Mahakama.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Kata ambazo zipo mbali na Makao Makuu ya Tarafa, ofisi yangu imeweka utaratibu wa kufanya assessment kutoka kwenye Makao Makuu ya Tarafa na itatoa upendeleo kwa Kata zile ambazo ziko mbali. Kwa hiyo, nina uhakika kabisa kwa sababu baada ya Bunge hili ziara yangu ya kwanza ni Kigoma, tutakwenda kuangalia hiyo na kuipa umuhimu unaostahiki.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Mahakama za Mwanzo hasa zilizopo Vijijini ambazo miundombinu yake imechakaa sana, ikiwepo Mahakama ya Gonja Maore, Jimbo la Same Mashariki katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuena kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mahakama nyingi za mwanzo zilijengwa katika mfumo ambao ni wa kizamani sana, na kwa sasa tunaendelea kuziondoa zingine katika sura kabisa ya Mahakama ulivyo sasa ili tujenge Mahakama nyingine nzuri zaidi. Kuhusu ukarabati kwa zile ambazo tunaziangalia kama zinaweza zikarekebika hizo ndizo tunaziwekea mpango wa kwenda kuzifanyia ukarabati na zoezi hilo linaendelea.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la Gonja, Mahakama za Mwanzo kama nilivyoeleza kwamba tutazipitia nazo kuangalia namna ambavyo tunaweza tukazifanyia kazi. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwenye bajeti iliyopita tulitengewa fedha kwa ajili ya kujenga Mahakama ya Wilaya ya Kyerwa lakini mpaka sasa Mahakama hiyo haijaanza kujengwa. Ni lini Serikali itaanza ujenzi ili kuondoa adha wanayoipata wananchi wa Wilaya ya Kyerwa.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; nipende kujibu swali la Mheshimiwa Bilakwate Mbunge wa Kyerwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba katika mpangokazi wa Wizara yangu tulipanga kuanzisha ujenzi wa Mahakama hii, iko kwenye mpango wa 2021/2022. Ninapenda tu kumuahidi kwanza Mheshimiwa Mbunge kwamba baada kikao hiki tutawasiliana kuona kama kuna uhakika wowote mradi huo haujaanza kwa sababu ofisi yangu haijapokea taarifa za kutoanza kwa mradi huu. Ahsante.

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 4

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Jengo la Mahakama ya Wilaya ya Nachingwea ni chakavu na limejengwa tangu enzi za wakoloni. Je, nini mpango wa Serikali wa kujenga jengo jipya litakaloendana na hadhi ya Wilaya?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Nachingwea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwamba ni kweli kama nilivyoeleza kwenye swali ambalo nimetoka kulijibu muda siyo mrafu, tunayo majengo ambayo yamechakaa lakini tunayo majengo ambayo yamekosa hadhi, kwa maana ya uhalisia wa miradi tuliyonayo kwa mwaka huu ambao unakwenda kumalizika tulikuwa tulikuwa na miradi 22, mwaka ujao tutakuwa na miradi 13 na inawezekana kabisa katika mwaka ujao ukawa umeingia kwenye mpango wa kuangalia uwezekano wa kujengewa Mahakama nyingine. Kwa hiyo, naomba tu Mbunge awe na utulivu katika kipindi hiki kwa sababu miradi yote mpaka kufikia 2025 tutakuwa tumekamilisha majengo yote ya ngazi ya Wilaya. Ahsante.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 5

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, asante sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali kupitia Mahakama zake imejenga Mahakama za Wilaya kwa kiwango safi kabisa. Je, ni lini Serikali itakamilisha kujenga Mahakama za Wilaya zote Tanzania kwa kiwango kama kile ambacho wameshajenga? ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma (Mshua) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza sehemu zote zenye Mahakama, zenye majengo ambayo yanaendelea kutumika hatuna mpango wa kwenda kuvunja na kuanza upya. Tuna mpango wa kujenga mahakama katika maeneo ambayo hayana mahakama kabisa lakini tutakarabati kwa kiwango bora zaidi kwenye yale majengo ambayo sasa yameendelea kutumika asante.

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria ameendelea kuyatoa kuhusiana na miundombinu ya Mahakama. Ningependa kuongeza taarifa ya uhakika kwamba Mahakama ya Tanzania ilishafanya utafiti wa hali ya miundombinu ya Mahakama nchi nzima kwa ngazi ya Mahakama za Wilaya, Mahakama za Mwanzo, Mahakama za Hakimu Mkazi na Mahakama Kuu. Kwa hiyo, upo mpango wa miaka mitano unaohusu ujenzi wa miundombinu ya Mahakama. Mpango ambao unaendana na mpango mkakati wa Mahakama ambao unaendana na kiasi cha fedha kilichotengwa kwa mahala ambako hakuna jengo la Mahakama kabisa, vilevile fedha iliyotengwa kwa Mahakama zinazohitaji ukarabati.

Mheshimiwa Spika, nitaomba labda Wizara ya Katiba na Sheria inachoweza kufanya ni kuwasilisha ule mpango ofisini kwako ili baadae mpango huo uweze kufikika kwa Waheshimiwa Wabunge wote. Pia tutaangalia uwezekano vilevile nakala kwa njia laini kama itawezekana ukaweza kuwa accessible na kila Mbunge. Nashukuru. (Makofi)

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Serikali iliahidi kujenga jengo la Mahakama katika Tarafa ya Heru, tarafa maalum ambayo alikuwa akiishi Mwami Theresa Ntare. Je, ni lini sasa Serikali itajenga jengo kumuenzi Mwami Theresa Ntare? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba tunapopeleka miradi kwenye maeneo mbalimbali tunapeleka kwa ajili ya mahitaji ya watu, sina uhakika sana kama tutakuwa tukipeleka kwa majina ya watu. Mimi ninapenda tu kumhakikishia kwamba eneo hilo kwa mahitaji yake tutakwenda kulipitia na kuona umuhimu wa kuweka hilo jengo lakini siyo kwa sababu aliishi mtu Fulani. Ahsate.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 7

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Jengo linalotumika katika Mahakama ya Wilaya katika Wilaya ya Meatu halikidhi hadhi kwa sababu lilikuwa ni Mahakama ya Mwanzo tukiwa Wilaya ya Maswa. Je, Serikali iko tayari kutujengea jengo jingine kwa kuwa eneo la kujenga Mahakama ya Wilaya tunalo?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali iko tayari kujenga jengo la Wilaya kama tu wanaendelea kutumia majengo ambayo hayakuwa mahsusi kwa ajili ya Mahakama za Wilaya. Kama tulivyoeleza hapo mwanzo tayari wako kwenye mpango na tutakapowasilisha ofisini kwako na kuwatumia wao wataona kila mtu kwenye position yake Mahakama yake inajengwa lini. Asante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kalambo ni miongoni mwa Wilaya ambazo hazina Mahakama za Wilaya na tayari kiwanja kilishapatikana kwa ajili ya ujenzi wa ujenzi wa Mahakama ya Wilaya. Je, Serikali ina kauli gani kwa ajili ya kujenga Mahakama katika Wilaya ya Kalambo?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephati Kandege Mbunge wa Kalambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika maelezo yangu ya utangulizi ni kwamba Serikali iko kwenye mkakati wa kujenga Mahakama za Wilaya na mradi huu utachukua kama alivyouleza AG unaishia 2025/2026. Kwa hiyo napenda tu kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba anakwenda kujengewa Mahakama ndani ya kipindi hiki nilichokitaja na nitawasiliana nae kumpa uhalisia wa mwaka ambapo tunapeleka mradi wake.

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 9

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi. Kwanza kabisa niwapongeze Serikali kwa kutujengea Mahakama Kuu nzuri na ya kisasa katika Jimbo la Shinyanga Mjini. Swali langu Mahakama ya Wilaya, Mahakama ya Mwanzo na Mahakama ya Hakimu Mkazi imechakaa sana, actually ilijengwa tangu kipindi cha ukoloni. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba Mahakama hizo zinakarabatiwa? Ahsante sana.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Makamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama tulivyoeleza katika mpango wetu kwamba tumetenga fedha za kukarabati majengo yote chakavu nchini na kujenga mapya katika maeneo yale ambayo yana uhitaji huo. Ninakuahidi tu Mheshimiwa Mbunge uvute subira kidogo utaona kazi inaendelea kule kwa ajili ya ukarabati.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 10

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kweli kuniruhusu na mimi niulize swali la nyongeza. Mahakama ya Wilaya ya Uyui inafanyakazi katika chumba kidogo kilichoazimwa kutoka kwa DC. Je, lini Serikali itajenga jengo la Mahakama ya Uyui?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maige Mbunge wa Uyuwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kule tuna mradi tayari unaendelea na tutafuatilia kuona unakamilika lini.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 11

MHE. ESTHER L. MIDUMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Itilima ni Wilaya mpya haina jengo la Mahakama.

Je, ni lini Serikali itajenga jengo hilo? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kwimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Kwimba ni Wilaya mpya na katika maelezo yangu ya utangulizi nimeeleza uhalisia wa mpango kazi ambao tunakwenda nao. Mimi nitapenda tu kuwasiliana nae baada ya kipindi hiki leo hii ili nimpe kalenda ya ujenzi utakavyoanza katika eneo lake la Kwimba. Ingawa katika mazingira ya kawaida Kwimba ipo katika mpango wa 2021/2022 program ambayo nina uhakika kabisa Kwimba kuna jengo linaendelea.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 12

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mahakama ya Wilaya ya Lushoto ni ya zamani tangia mkoloni. Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati au kujenga Mahakama mpya Wilayani Lushoto?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi Mbunge wa Lushoto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Lushoto nilifanya ziara hivi karibuni na tayari wataalam walishafanya assessment juu ya ukarabati ule. Kwa hiyo, muda wowote jengo lile la Wilaya linaweza likaanza ukarabati. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Buhigwe ili wananchi waweze kupata huduma?

Supplementary Question 13

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza nishukuru Serikali kwa kujenga Mahakama ya Hydom imekamilika kabisa. Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri mnafungua Mahakama ile ya Hydom ili ipate kutumika?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Hydom tayari jengo limeshakamilika na utaratibu wa matumizi unaweza ukaanza wakati wowote. Lini tutakwenda kuzindua rasmi ni mpango wa Mahakama ambao huwa wana utaratibu ambao wanautumia katika kwenda kuzindua na uanzishwaji wa matumizi ya Mahakama. Juzi Waziri wangu alikuwa pale Hydom kuangalia hilo jengo na nina uhakika kabisa Mheshimiwa Mbunge alikubaliana jambo na Mheshimiwa Waziri. Ahsante. (Makofi)