Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Wodi ya Akinamama, Watoto na Wanaume katika Vituo vya Afya Lukungu - Lamadi na Kiloleli?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE; Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Kata hizi mbili ambazo nimezitaja na vituo vya afya ambavyo nimevitaja vina wananchi wengi na vinahudumia wananchi wengi sana katika vituo hivi.

Je, Serikali sasa haioni sababu za kuwa na mpango wa haraka ili kuharakisha ujenzi wa wodi hizi ambazo nimezitaja ili wananchi waweze kupata huduma wasisafiri umbali mrefu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, ni kweli Kituo cha Afya cha Lukungu na Kiloleli ni miongoni mwa vituo vya afya ambavyo vinahudumia wananchi wengi sana na kwa kutambua hilo, tayari Serikali imekwishaainisha vituo vya afya vyote ambavyo vina miundombinu pungufu na vinahudumia wananchi wengi ili fedha iweze kutafutwa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunaongeza miundombinu ambayo inapungua.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Songe kwamba Kituo cha Afya cha Lukungu tayari kimeingizwa kwenye mpango huo na mara fedha ikipatikana tutahakikisha tunaenda kujenga miundombinu hiyo, ahsante