Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, je, ni lini sasa Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati katika Kata ya Binza Kijiji cha Iyogero?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, ni lini Serikali itapeleka fedha za kukamilisha kujenga zahanati katika Kijiji cha Ng’hami Wilaya ya Maswa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafuatilia kuona hatua ambazo majengo haya ya zahanati yamefikia ili tuweze kuweka kwenye bajeti kwa ajili ya kukamilisha majengo haya, ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ni lini atapeleka fedha katika Zahanati ya Tiling’ati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli Zahanati ya Tiling’ati tulifika pale na wanahitaji shilingi milioni kumi kwa ajili ya ukamilishaji na Mheshimiwa Waziri wa Nchi alishaahidi kwamba fedha zitakwenda pale. Namhakikishia kwamba tutafuatilia kuhakikisha kwamba shilingi milioni kumi zinapelekwa pale Zahanati ya Tiling’ati, ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, tatizo la maboma ya zahanati nchi nzima imekuwa kero na ya muda mrefu tangu 2010, je, Serikali imefanya utafiti ni yapi yanaweza kutengenezeka?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni kweli, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba kumekuwa na maboma mengi katika vijiji vyetu kwa ajili ya zahanati lakini kwa kweli katika kipindi cha miaka hii mitatu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amekamilisha maboma zaidi ya 900. Kwa hiyo, kazi ya Serikali ni kuendelea kutambua maboma ambayo tayari yanakidhi vigezo vya kukamilishwa na fedha zinaendelea kutengwa. Mwaka huu wa fedha shilingi bilioni 90 zimetengwa kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma hayo.

Mheshimiwa Spika, tunafanya utafiti na tutaendelea kuyakamilisha kwa awamu, ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 4

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kulingana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, anaonesha kwamba wananchi wanapaswa kuchangia ujenzi wa zahanati hadi kwenye maboma, lakini wapo watu ambao wamekuwa wakipita kwenye majimbo yetu wakiwaambia wananchi wasichangie ujenzi wa zahanati na maboma mengine ya elimu: Je, nini hatua ya Serikali dhidi ya hao ambao wanapotosha wananchi wasishiriki mendeleo yao? (Makofi

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Utaratibu wa ujenzi wa maboma ya zahanati kwa mpango wa maendeleo ya afya msingi upo kwa mujibu wa mwongozo wa 2007. Ni maamuzi ya Serikali kwamba wananchi wanashiriki kwa sehemu na Serikali inahitimisha. Kama wapo watu ambao wanapita katika maeneo yetu na kupingana na maelekezo ya Serikali basi naomba Serikali kwa maana ya Wakurugenzi, Wakuu wa Wilaya na Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa wawatambue watu hao ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao, ahsante. (Makofi

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 5

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Jimbo la Rungwe, wananchi wameweka nguvu sana katika kujenga maboma ya zahanati, ni lini Serikali itaongeza fedha ili kuweza kumalizia maboma hayo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Serikali imekuwa ikitenga fedha kila mwaka kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma na ninafahamu Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe imepata fedha zaidi ya shilingi milioni mia tatu kwa ajili ya maboma sita ya zahanati katika kipindi cha miaka miwili. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma hayo.

Mheshimiwa Spika, pia nawakumbusha Wakurugenzi na Makatibu Tawala wa Mikoa kwamba tulitoa maelekezo lazima tuwe na uratibu wa ujenzi wa maboma badala ya kila mtu kuamua kila siku kujenga boma na mwisho wa siku maboma yanakaa muda mrefu. Wazingatie utaratibu huo kwa maana kuratibu na Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya umaliziaji, ahsante. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Lini Serikali itaanza mchakato wa ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Likawage, Jimbo la Kilwa Kusini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Kata ya Likawage katika Wilaya ya Kilwa inahitaji Kituo cha Afya na Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia mara kwa mara. Tulishaelekeza wataalamu kwa maana Mganga Mkuu wa Wilaya na Mganga Mkuu wa Mkoa, wafanye tathmini ya vigezo na kuwasilisha maombi Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Nasisitiza tupate taarifa hiyo ndani ya wiki mbili ili Mheshimiwa Waziri wa Nchi aweze kuona uwezekano wa kupeleka fedha kwa ajili ya ujenzi huo, ahsante.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 7

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni lini Serikali itakamilisha Kituo cha Afya cha Migori kilichopo Kata ya Migori ambacho kimejengwa na nguvu za wananchi karibu takribani shilingi milioni 10.8 ambazo wamechangia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kutumia fursa hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa waweze kuwasilisha maombi hayo ili tuweze kuona kama inakidhi vigezo tuweze kupeleka fedha kwa ajili ya ukarabati na ukamilishaji wa jengo hilo.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 8

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini Serikali itatupatia fedha ili tuweze kujenga Kituo cha Afya katika Tarafa ya Nangaru?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, hivi sasa tayari Serikali imeanza kufanya tathmini ya pili ya tarafa ambazo hazikupata vituo vya afya vya kutosha kwa awamu ile ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati tunaendelea na tathmini hii, tutatoa kipaumbele katika Kata hii ya Nangaru kuona uwezekano wa kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya uweze kutekelezwa. Ahsante.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Zahanati katika Kata ya Binza – Maswa?

Supplementary Question 9

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Ni lini sasa Serikali itatoa commitment ya kuibadilisha Zahanati ya Town Clinic Tabora Mjini na kuwa kituo cha afya kwa sababu inazalisha watu wengi kwa mwezi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Town Clinic katika Manispaa ya Tabora ni zahanati ya muda mrefu na inahudumia wananchi wengi sana. Serikali ilishatoa maelekezo kwa Mkurugenzi, walishaelekezwa kuandaa michoro ya ghorofa kwa sababu eneo lile ni dogo ili fedha ziweze kutengwa kwa ajili ya kujenga ile zahanati na kupandisha hadhi kuwa kituo cha afya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, natumia fursa hii kumkumbusha Mkurugenzi na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, kutekeleza maelekezo ya Serikali mapema ili tathmini ifanyike, fedha zitafutwe kwa ajili ya kupandisha hadhi zahanati hii kuwa kituo cha afya. Ahsante. (Makofi)