Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA aliuliza: - Je, ni lini majimbo ya Zanzibar yatapata fedha za Mfuko wa Jimbo kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini ningependa kujua: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na Maafisa Maalum walio chini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watakaokuwa wanasimamia fedha hizi kwa upande wa Zanzibar badala ya kutegemea Maafisa wa Serikali ya Mapinduzi ambao hawawajibiki moja kwa moja katika Bunge letu?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdul-hafar Idrissa Juma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali hilo, kwa ruhusa yako naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Abdul-hafar kwa namna anavyopigania Mfuko wa Jimbo kwa Jimbo lake na majimbo mengine ya Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, Sheikh Abdul-hafar swali lako kama ushauri tumelichukua tunakwenda kushauriana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tuone kama ufanisi utapatikana zaidi kwa kuweka Maafisa kule basi Serikali yako ni sikivu na inaweza ikafanya hivyo. (Makofi)