Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa kuwa Wilaya ya Kwimba ndiyo Wilaya pekee katika Mkoa wa Mwanza ambayo haijaunganishwa kwa barabara ya lami na Makao Makao Makuu ya Mkoa wa Mwanza, na Wilaya Kwimba ni miongoni ya Wilaya kongwe imeanzishwa toka mwaka 1935. Sasa angalia mpaka muda huu haijawahi kuunganishwa na barabara ya lami.

Je, ni lini Serikali itakamilisha kilomita 25 za kutoka Mwabuki kwenda Ngudu mjini ili Wananchi wa Wilaya ya Kwimba waweze kuungana na Mkoa wa Mwanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la nyongeza la pili ni kwamba, kwa kuwa barabara yetu ya Mwabuki, inaunganisha pamoja pamoja na Barabara ya Malampaka – Maswa ambayo ni katika Mkoa wa Simiyu na barabara hiyo ni ndefu inakwenda mpaka Singida. Je, ni lini Serikali sasa itakamilisha ujenzi wa barabara hiyo? kwa sababu ya kupunguza traffic kubwa kati ya Mwanza na Singida kwa njia ya shortcut ya kupitia Maswa, Meatu pamoja na Singida, ahsante. (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Tabasam, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi. Tunajenga hizi kilomita 28 na tumeanza na kilomita tatu, kuanzia Ngudu ambako ndiyo Makao Makuu ya Wilaya lakini vilevile kwa Barabara ya Magu – Ngudu tumeanza kujenga kilomita 10 kutoka Magu kwenda Ngudu. Kwa hiyo mtandao huu utaunganisha Wilaya ya Kwimba na Mwanza kwa maana ya Mwanza mjini, kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Tabasam na Mheshimiwa Mansoor kwamba maendeleo ni hatua tumeanza hivyo lakini nia ni kuiunganisha Wilaya ya Kwimba pamoja na Mwanza, kwa maana ya Mwanza mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile kuhusu swali la pili Mwabuki - Maswa; sasa hivi Serikali ipo kwenye Miradi saba ya EPC+F ipo barabara yenye kilomita 389 ambayo inaanzia Mbulu kuja Manyara, Singida mpaka Maswa. Barabara hii inaenda kuunganisha Mikoa ya Kaskazini pamoja na Kanda ya Ziwa na ikishafika pale Maswa na mitandao hii ambayo nimeitaja tutakuwa tumeunganisha mikoa ya Mwanza, Simiyu, Singida na Mikoa ya Kaskazini, ahsante sana. (Makofi)

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mwaka jana tarehe 16 Juni, tulisaini Mikataba ya Barabara za EPC+F ya Kongwa – Kiteto – Arusha. Naomba kufahamu lini Mradi huu unaanza kwa sababu Wananchi wa Kiteto tunausubiri kwa hamu sana?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Olelekaita, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili nilijibu kwa package yote ya miradi yote ya EPC+F, miradi saba. Kama nilivyosema wakati nachangia kwenye hoja ya Kamati ya Miundombinu, design ya barabara hizi ilifanywa na TANROADS mwaka 2017 miaka mingi imepita. Kwa hiyo Wakandarasi ambao wamepatikana wanafanya mapitio ya design ili kuweza ku-update usanifu wa kina, na baada ya hapo barabara hizi zitaanza kujengwa mara moja. Kwa hiyo nimuombe Mheshimiwa Olelekaita pamoja na Waheshimiwa Wabunge ambao mnasubiri hii Miradi ya EPC+F tuko tunajipanga usanifu, mapitio yakikamilika basi tutaanza ujenzi wake, ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa kuwa taratibu zote za Ujenzi wa Kipande cha Barabara kati ya Nansio – Lugezi – Kisolya umekamilika lakini Mkandarasi hajafika site. Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya mradi huu?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Jimbo la Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia barabara hii tumepeleka hazina yapo masuala ya VAT lakini nimhakikishie nitakaa na Kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba ili maombi ambayo tumeyapeleka ya VAT waweze kutukamilishia na ujenzi wa barabara hii uweze kuanza mara moja. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa Namtumbo tuna barabara ambayo inatoka Makao Makuu ya Wilaya inapitia katika Kata ya Likuyu, Mgombasi inaunganisha mpaka kwenye Kata ya Kitanda. Kuna daraja ambalo ni la zamani sana lipo katika Mto Uwegu ambalo katika mvua hizi limesukumwa hilo daraja na kufanya kuhatarisha maisha ya Wananchi na vyombo vyao. Je, Serikali iko tayari sasa kuiweka kwa dharura bajeti ya kutengeneza daraja hili la Mto Uwegu ambalo linaunganisha Kata ya Namtumbo, Likuyu na Mgombasi? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kawawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kuwa Mheshimiwa Kawawa ameishakuja kuniona kuhusu daraja alilolitaja. Nimeona video na namna ambavyo mawasiliano yamekatika. Nitumie nafasi hii nimuagize Meneja wa TANROAD Mkoa wa Ruvuma kuwasilisha mahitaji ya daraja la dharula katika hili eneo ambalo Mheshimiwa Kawawa alinionyesha ili tuweze kumpelekea daraja la dharula la chuma, ahsante sana. (Makofi)

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Mbinga – Muyangayanga – Mahenge – Litembo ina urefu wa kilometa 25. Ninaishukuru Serikali imejenga vipande vya lami kwenye maeneo korofi.

Je, ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema tumeanza kujenga maeneo korofi. Nimhakikishie kwamba kadri fedha zitakapokuwa zinapatikana tutaendelea kuboresha maeneo ambayo yanahitaji kudhibitiwa, ahsante sana.

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini sasa Serikali itajenga barabara inayotoka Mtwara mjini kuelekea Msimbati ambako kuna visima na mitambo ya gesi kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shamsia, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua jambo hili kwenye Ziara ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan wewe pamoja na Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Mtwara mliliulizia na maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni barabara hii ni ya muhimu. Kwa hiyo tunaendelea kujipanga kadri fedha zitakapopatikana tutaijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Tangu mwezi Juni, mwaka jana tumesaini Mkataba wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mnivata – Newala – Masasi. Je, ni lini ujenzi huu utaanza? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Chikota ameulizia barabara hii ni sehemu ya ile miradi ya barabara za EPC+F. Kama nilivyoeleza, tuko hatua za mwisho za mapitio ya usanifu wa kina ili ujenzi wa barabara hizi uweze kuanza ikiwemo hii barabara ambayo Mheshimiwa Chikota ameuliza.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Barabara ya Bujera – Masukulu – Matwebe hadi Kyela ni barabara muhimu sana kiuchumi katika Wilaya ya Rungwe. Ni lini Mheshimiwa Waziri utatusaidia ili barabara hii iwe katika kiwango cha lami?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwakagenda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii tutaijenga kama tulivyoipanga kwenye bajeti, kile ambacho tumeweka kwenye bajeti nikuhakikishie tutakizingatia na kama hakipo basi tutajitahidi kujenga barabara hii kadri bajeti itakavyoturuhusu kwenye hizo bajeti zijazo, ahsante sana.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, ni nini, kauli ya Serikali katika kuipanua barabara ya Dar es Salaam hadi Dodoma kutokana na ufinyu wake na matumizi makubwa ya barabara hii.

Je, Serikali haioni haja ya kuipanua barabara hii na kuifanya njia nne?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru kwa ufatiliaji wake, Dodoma ni Makao Makuu ya nchi na Dar es Salaam ndiyo Commercial City ya nchi yetu, kwa hiyo, ni vizuri tukaviunganisha kwa mawasiliano ya barabara ya uhakika. Bahati nzuri kama nilivyosema juzi, kwenye hoja za Kamati ya Miundombinu, tunapanga kujenga barabara hii ya kutoka Kibaha inapoishia njia nane, Chalinze, Morogoro mpaka Dodoma kutumia utaratibu wa PPP.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari wapo wabia ambao wamejitokeza tunaendelea na mazungumzo nao, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Tarimba pamoja na Waheshimiwa Wabunge kwa sababu wote tunahitaji barabara hii kuunganisha Dar es Salaam pamoja na Dodoma, tuko mbioni kuijenga barabara ya Express Way Dar es Salaam – Dodoma kwa njia ya PPP, ahsante sana.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, treni ya mwendokasi kutoka Dar es Salaam ndani ya miezi michache itaanza kufanya kazi na kuna uwekezaji mkubwa kwenye kituo cha treni pale Kilosa, wakati huo huo kuna uwekezaji zaidi ya dola milioni 120 kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mikumi ambayo inaenda kuongeza ndege mpaka 50 kwa siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokukamilika kwa barabara ya kutoka Kilosa kuja Mikumi kuunganisha miundombinu hii miwili muhimu sana kwa Taifa letu; je, ni amri, taaluma au utaalamu?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Londo, nimhakikishie barabara hii ni muhimu na Serikali inafanya kila jitihada lakini yote haya yanategemeana na upatikanaji wa fedha. Kwa hiyo, nimhakikishie fedha zitakapopatikana tutaweka barabara hii kuijenga kwenye utaratibu aliouomba. Nakushukuru sana.

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 11

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi; ni lini, Serikali itatekeleza ahadi ya Makamu wa Rais kujenga barabara ya lami kutoka kipande cha Ngaresero mpaka Engaruka kilomta 39?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Ole-Shangai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa amekuwa akifuatilia barabara hii na ahadi za Viongozi wetu ni maelekezo, tayari barabara hii tumeiweka kwenye kupaumbele. Kwa hiyo, nimhakikishie tutakapopata fedha barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami.