Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa, tarehe 7 Agosti, 2022 Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alipotembelea pale Rungwe Serikali ilitoa ahadi kwamba mradi huu ungekamilika mwezi Oktoba, 2023; na kwa kuwa, tarehe hiyo imepita sasa; je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza akawaeleza wananchi wa Tukuyu kwamba ni lini sasa mradi huo utakamilika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Mradi wa Maji uliopo Wilaya ya Mwanga, Kata ya Kileo, sehemu inaitwa Mnoa, ambao unakusudia kuwahudumia wananchi wa Vijiji vya Kileo, Kituri na Kivulini, wenye thamani ya shilingi bilioni 1.3; je, ni lini sasa mradi huu utakamilika ili wananchi wa vijiji hivi vitatu vya Kileo, Kituri na Kivulini, Kata ya Kileo waweze kupata maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Albert Anton Mwantona, kwa niaba yake limeulizwa na Mheshimiwa Joseph Tadayo, lini mradi huu utakamilika; kipande ambacho tulimwahidi Mheshimiwa Rais kukamilika, kilishakamilika. Ni hizi kilometa tisa kutoka kule kwenye chanzo cha Mto Mbaka mpaka pale kwenye tanki. Ni mimi mwenyewe kabla ya ule mwezi wa Kumi nilikwenda pale Tukuyu na tukahakikisha maji yameweza kuingizwa kwenye existing line.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo ambalo limebaki kama nilivyosema, kufikia mwezi Aprili tunatarajia tanki liwe limekamilika lijazwe na kuongeza uzambazaji kwa existing line na kuongeza line mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile kwenye swali la pili la kutoka Mwanga, Mradi wa Moa, huu mradi umekamilika kwa asilimia zaidi ya 95 na tayari maeneo ambayo yanapitiwa na mradi huu yanaendelea kukamilishwa, na mwezi huu Februari tunatarajia maji yaweze kufika kwenye vijiji hivi alivyovitaja vya Kileo na Kivulini. Kwa watu wa Kituri, wenyewe kwa sasa hivi wanapata maji kutoka kwenye Mradi wa Kifaru. Kwa hiyo, wapo kwenye mpango wa kuongezewa extension kutoka kwenye huu Mradi wa Mnoa, baada ya hawa ambao hawana maji kabisa kupata, nao watapelekewa maji vilevile. (Makofi)

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana; bei ya maji pale Same sasa hivi ni kati ya shilingi 4,000 mpaka shilingi 5,000 kwa ndoo na adha hii inawakumba sana wanawake wa Same; ni lini sasa Mradi wa Mwanga – Same – Mombo utakamilika ili waweze kupunguza adha hii?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa mama yangu kuhusu Mradi wa Same – Mwanga – Korogwe; mradi huu kwa sasa hivi tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais, ameweza kutuwezesha na wakandarasi wote kwenye kila kipengele wapo kazini. Kufikia mwezi Juni, 2024 tunatarajia mradi uwe umekwisha. Mpaka leo hii mradi upo asilimia 86.