Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA K.n.y. MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, lini Mkoa wa Rukwa utaunganishwa na Gridi ya Taifa ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri, nami nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza: Je, ni mikoa mingapi hapa nchini hadi sasa haijaunganishwa na Gridi ya Taifa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Nafahamu kwamba Kigoma nayo ipo katika mpango wa kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia vituo vya Urambo na Ipole Sikonge. Sasa swali ni kwamba wananchi watalipwa lini fidia kwenye ile njia ya kutoka Tabora kwenda Ipole?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kakunda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na mikoa ambayo haijaunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, mikoa miwili ya Katavi na Rukwa ndiyo ambayo haijaunganishwa kabisa kwenye Gridi ya Taifa. Mikoa ya Mtwara, Lindi, Kigoma na Kagera imeunganishwa kidogo kwa Msongo wa kilovolt 33, lakini miradi inaendelea ili tuiunganishe kwa Msongo Mkubwa wa Kilovolt 220 na Kilovolt 400. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na fidia ambayo ameuliza Mheshimiwa Mbunge, tayari tumeshafanyia kazi na tunategemea ifikapo tarehe 30 mwezi huu wa Novemba, 2023 wananchi wataanza kulipwa, ahsante.