Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, lini Serikali itamaliza mgogoro wa ardhi kati ya mwekezaji wa Shamba la Malonje na wananchi wa Kata ya Muungano na Mollo Kwela?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa ya swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Bunge la Bajeti lililopita Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata aliuliza swali juu ya mgogoro huu na ulitoa maelekezo kwamba Waziri afanye utaratibu wa kuja kuangalia mgogoro huu na umalizike. Hata hivyo, nashukuru Naibu Waziri alikuja, jambo lililofanyika ni kutoa maelekezo kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wahakikishe wanashughulikia tatizo hili. Mheshimiwa Naibu Waziri hakupata fursa ya kwenda field kuona tatizo na uhalisia wake.

Mheshimiwa Spika, naomba tena nirudie, naomba tena kupitia Bunge lako, niombe Waziri aje Mkoa wa Rukwa, aende akafuatilie aone uhalisia wa tatizo hili kwa sababu suala la kumuachia Mkuu wa Mkoa limekuwepo tangu miaka 13 iliyopita ambapo Mkuu wa Mkoa, mama yangu Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya analijua vizuri. Ninataka Waziri aje na timu ya wataalam wajifunze vizuri kuliko haya majibu ambayo yanaweza yakachochea hasira na mgogoro zaidi, nakushukuru. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini niungane na Mheshimiwa Mbunge kwa concern yake ya kupambania wananchi wake.

Naomba nimuahidi tarehe 17 Novemba, baada tu ya Bunge hili nitafika jimboni kwake, nikiambatana na timu ambayo tumeunda task force ya wataalam kwa ajili ya kutatua migogoro mikubwa kama hii, kwenda uwandani kuona hali halisi na kutatua tatizo hili mara moja, ahsante sana. (Makofi)