Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati ghala la mazao lililopo katika kata ya Ludewa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza; na nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa na kawaida wakati fulani kuzuia mahindi ya Tanzania kuuzwa nje ya nchi, jambo ambalo linaadhiri sana bei ya zao hili la mahindi kwa wakulima.

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba mahindi ya Tanzania yanaruhusiwa kwenda kuuzwa nje ya nchi ili wakulima wapate bei nzuri?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; bei za mbegu za mazao mbalimbali zimekuwa zikipanda kwa kasi sana.

Je, Serikali ina mpango gani walao kwa kuanzia na zao la mbegu za mahindi, Serikali ina mpango gani wakuweka ruzuku kwenye bei ya mbegu ya mahindi ili wakulima waache kurudia mbegu au kutegemea mbegu za asili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo la kwanza, nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa maswali yake ya msingi. Nimuondoe shaka kwamba moja ya wajibu wetu sisi kama Wizara ya Kilimo tunapokuwa tunazuia wakati fulani mahindi kuuzwa nje ya nchi lengo letu linakuwa kwanza, kujiridhisha kupata tathmini halisi ya usalama wa chakula nchini; na tunafanya hivyo ikiwemo kwa kutumia wakala wetu wa hifadhi ya chakula nchini kununua. Tukishamaliza jambo hilo ndipo ambapo huwa tumekuwa tukiruhusu wananchi kufanya biashara. Kwa hiyo tunaendelea kulizingatia ili kuleta namna bora ambayo itasaidia soko kwa wakulima wa mahindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuweka ruzuku katika bei ya mahindi, kwa maana ya mbegu mbalimbali ikiwemo mahindi, jambo hilo tumelipokea. Ndiyo maana katika mipango yetu ya awali, mwazo tumeanza na ruzuku katika upande wa mbolea na pembejeo nyinginezo zikiwemo viuwatilifu; lakini next maana yake tutakuja katika pembejeo nyinginezo zikiwemo bei za mahindi. Kwa sasa tumeanza na hizo items mbili then tutakuja katika hilo jambo lingine. Kwa hiyo, hilo tumelipokea na lipo katika mipango yetu. Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati ghala la mazao lililopo katika kata ya Ludewa?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa pale Vwawa eneo Isangu kuna maghala yalikuwa yanajengwa na Serikali ambayo yametelekezwa; na tangu mwaka 2020 mkandarasi aliondoka akaacha ule mradi.

Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba maghala yale ambayo ni ya kisasa kwa maana ya vihenge yanatekelezwa ili yaweze kuchangia katika uchumi wa taifa letu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mpango wa Serikali kwa Maghala ya Vwawa na maeneo mengine yakiwemo yale ya Songea ni kwamba tulishawapa kazi NFRA kufanya tathmini halisi ya gharama ya maghala yote nchini, kuhakikisha tunayamaliza katika mwaka wa fedha unaokuja kwa kutumia fedha zetu za ndani. Huo ndiyo mpango wetu, kwa sababu lengo la Serikali ni kuongeza uhifadhi wa chakula kutoka tani laki 3 za sasa walao mpaka mwakani tuende kwenye tani laki saba na mwaka 2030 tufikie tani milioni tatu. Kwa hiyo mpango tulionao wa muda mfupi ni kuyamaliza yote kwa fedha za ndani.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati ghala la mazao lililopo katika kata ya Ludewa?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Soko la Kimataifa ya Mazao la Lemagu ambalo lipo mpaka wa Sirali ni soko la kimkakati katika kukuza uchumi wa Taifa letu. Soko hilo lilijengwa na kutelekezwa zaidi ya miaka 12 iliyopita; na katika kufuatilia Serikali iliahidi kulifufua. Nataka kujua mchakato umefikia hatua gani katika kufufua soko lile?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, bahati nzuri hili soko mimi nalifahamu. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba alishapatikana mkandarasi anaitwa Nice Construction. Soko hilo litagharimu karibu bilioni 1.04 kwa ajili ya kulijenga na kulimaliza. Kwa hiyo hatua ipo vizuri na kazi itaendelea muda mfupi.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati ghala la mazao lililopo katika kata ya Ludewa?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsnate. Wananchi wa Kijiji cha Kambi ya Simba Kata ya Bulumbulu wamejenga ghala kubwa ya kuhifadhia mazao yao lakini halijakamilika.

Je, lini Serikali itaweza kwenda kukamilisha lile ghala iliyopo katika Kijiji cha Kambi ya Simba?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika swali la awali. Ni kwamba NFRA wamefanya tathmini ya maghala yote nchini na wameshatupatia hiyo taarifa, tunachokifanya sasa hivi sisi tunatafuta fedha na maghala yote nchini tutamaliza kwa fedha za ndani, likiwemo ghala hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amelisema.