Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza tatizo la mimba za utotoni kwa watoto wa kike?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, nini mkakati wa Serikali kushirikisha taasisi mbalimbali zinazojihusisha na elimu ya masuala ya afya ya uzazi. Je, Serikali haioni haja ya taasisi hii kupata vipindi kwenye mashule mbalimbali ili kutoa elimu kwa watoto wa kike?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa vile mimba za utotoni zinaenda sambamba na ndoa za utotoni. Nini sasa baada ya Serikali kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali. Lini Serikali italeta Muswada wa ndoa za utotoni?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Janeth, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na wadau tunaimarisha mikakati ya uratibu za afua na kutoa huduma za afya shuleni kwa kushirikiana na majukwaa ya watoto walioko shuleni, vitabu vya watoto, madawati, ulinzi na usalama, mabaraza ya watoto, na kutumika katika elimu ya afya shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili. Wizara ya Maendeleo ya Jamii ikishirikiana na Wizara ya Katiba na Sheria inaendelea na mchakato wa kukusanya maoni juu ya kujua umri wa kuolewa kwa mtoto wa kike. Pia, mchakato huo ukimalizika Muswada huu utaletwa katika Bunge lako Tukufu na kujadiliwa na kupitishwa sheria ya kuthibiti ndoa za utotoni.