Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha uchimbaji wa visima vya maji vilivyoanza kuchimbwa katika Jimbo la Buchosa?

Supplementary Question 1

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali.

Swali la kwanza, ni kweli kwamba visima hivi vimechimbwa, lakini kwa hivi sasa vimesimama na hakuna fedha ya kuendeleza. Je, Serikali italeta lini fedha ili kukamilisha uchimbaji wa visima hivyo?

Swali la pili, mradi wa maji kutoka Kijiji cha Lumeya, Nyakalilo, Kalebezo, Mizolozolo mpaka Nyehunge haufanyi kazi ipasavyo kwa sababu mambomba yake yanapasuka. Je, Serikali iko tayari pia kuukarabati mradi huu ili uweze kufanya kazi kwa ukamilifu wake? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, lini fedha itakwenda kwa ajili ya kuendeleza visima. Tayari Mheshimiwa Waziri ametoa maagizo kwa Mameneja wa Mikoa wote kuhakikisha hivi visima vinaweza kuendelezwa na tija ya uchimbaji visima hivi kunaweza kupatikana kwa maji bombani kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukarabati mradi ambao umekamilika lakini mabomba yanapasuka, hapa kwanza tumshukuru Mheshimiwa Rais, kwa kutupatia fedha na kuhakikisha miradi inakamilika. Unapoona mabomba yanapasuka maana yake maji yamekuwa ni mengi tofauti na ilivyokuwa nyuma. Kwa hiyo, tuko tayari kukarabati ili kuhakikisha maji mengi yaliyopatikana sasa yanawafikia wananchi. (Makofi)