Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: - Je, lini miundombinu ya mipaka ya nchi yetu itaboreshwa ili kukuza diplomasia ya uchumi na nchi zenye fursa za kibiashara kama DR – Congo?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni miaka miwili sasa bandari ya Kalema ipo tayari lakini hakuna tija iliyopatikana licha ya Serikali kuwekeza zaidi ya bilioni 47. Hii inaleta shida kwa sababu fedha za wananchi zimekaa pale na hakuna pesa inayopatikana kwa sababu tu ya ubovu wa miundombinu ya barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka commitment ya Serikali ni lini exactly barabara hii ya kutokea Kigwira kuelekea Karema, itatengenezwa ili kuokoa fedha za walipakodi? (Makofi)

Swali la pili, tuna barabara za kimikakati kuzunguka nchi za SADC. Ni lini, Serikali itaainisha barabara hizi, ili kuweza kuweka soko pamoja lakini kuokoa fedha zinazopotea na kikubwa zaidi kuongeza pato la mtu mmoja mmoja na la Taifa? Ahsante. (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Felista Njau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi barabara ambayo Mheshimiwa Felista ameitaja ya Kigwira kwenda Karema, tumeshasaini mkataba, kwa hiyo, baada ya kusaini ina maana Mkandarasi anaanza ku-mobilize mitambo ili ujenzi wa kiwango cha lami uweze kuanza. Vilevile Serikali ya Awamu ya Sita hatujaishia hapo, dhamira ya Serikali Tanzania ni sehemu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Tanzania ni sehemu ya Jumuiya ya SADC pia kuna African Union 2063 (The Africa We Want).

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha position ya Tanzania katika mikakati ya kiuchumi kwenye jumuiya hizi nilizozitaja, EAC, SADC na AU - Vision ya 2063 (The Africa we want). Tanzania tunataka tujipange tuwe vinara wa kiuchumi. Kwa hiyo, ujenzi wa barabara hizi na nchi za jirani siyo kwamba tunajenga tu kwa sababu tunawapenda sana, ndiyo ni mahusiano mazuri pia kimkakati lazima tuji-position ili kuweza kujenga uchumi imara, kutengeneza ajira kwa wananchi wetu na kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Kwa hiyo nikuhakikishie mikakati yote tunayo na tunaendelea kuitekeleza, ahsante sana. (Makofi)