Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, utaratibu gani unaotumika kwa Kamandi mbalimbali nchini kuanzisha miradi ya kibiashara katika maeneo ya Kamandi?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na nimpongeze sana kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kama mnavyojua kwamba, baadhi ya Kamandi au Kambi kumekuwa na tabia ya ukataji wa miti na uondoaji wa misitu ambayo imekuwepo kwa muda mrefu. Sasa, nilikuwa naomba tu kujua Mheshimiwa Waziri, wana mwongozo gani wa kushirikiana na Taasisi za Idara za Mazingira na Misitu hasa kule Zanzibar, ili kuona kwamba miradi hii ikiibuliwa na ikitekelezwa basi haiathiri mazingira?

Swali namba mbili, je, Kamandi au Wizara ina utaratibu gani wa kuwa na mwongozo wa mapato na matumizi kama vile walivyo wenzetu wa Jeshi la Polisi ule mpango wa Tuzo na Tozo, ili kuhakikisha kwamba, mapato yanayopatikana yanatumika katika njia ya ufanisi zaidi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, miradi hii huzingatia pia taratibu za uhifadhi wa mazingira. Kwa hiyo, tunafuata mwongozo wa Serikali kuhakikisha kwamba, taratibu za uhifadhi wa mazingira zinazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mwongozo wa mapato na matumizi; Miradi hii inaendeshwa kwa kuzingatia kwanza inachambuliwa na Makao Makuu ya Jeshi na umewekwa utaratibu ambao pesa zote zinazopatikana zinafuata Taratibu za Matumizi ya Fedha katika Taasisi za Umma. Kwa hiyo, hakuna wasiwasi kwamba, pesa hizi labda zinapotea na nipende kutoa pongezi kubwa sana kwa Jeshi letu la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, kwa kazi kubwa mabyo wameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kipindi tulikuwa na ukwasi lakini miradi hii imesaidia katika kutekeleza majukumu ya msingi ya Jeshi. Kwa hiyo, nawapongeza sana Jeshi letu na nikuhakikishie kwamba, taratibu na matumizi ya fedha haya yanafuata taratibu zote, hata audit huwa zinafanywa, ahsante sana.