Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza kuunganisha mita za maji za kulipia kabla ya matumizi kama za TANESCO Arusha Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia majibu ya Serikali, yanaonesha kwamba zoezi hili lilianza mwaka 2019 na mpaka leo ni takribani miaka mitano, wameweza kufungia wananchi 345 ambayo ni sawa na asilimia 0.285 kwa miaka mitano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizingatia kwamba wananchi wa Jimbo la Arusha Mjini wamekuwa wanalalamika kwa muda mrefu sana kuhusiana na bili kubwa za maji na kubambikiwa bili; je, nini kauli ya Serikali kuhusiana na changamoto hii? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ni kwamba, kama kwa miaka mitano tumeweza kufungia wananchi kwa maana ya 345 kati ya wananchi 120,899 ambao wanatakiwa kufungiwa mita za LUKU za namna hiyo; je, Serikali imejipangaje kuweka timeframe kuhakikisha kwamba wananchi wote 120,899 wanafungiwa mita za maji kama za LUKU?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mrisho Gambo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kujipanga kuhusiana na ubambikaji wa bili kwa wananchi, hili tayari tumeshalifanyia kazi kubwa sana. Zoezi hili limeanza taratibu kwa sababu ya kutoa elimu na kuhakiki hizi dira ambazo tumekuwa tukizitoa nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba tumejipangaje sisi kama Wizara, tayari tumetoa fursa kwa vyuo vyetu vya ufundi hapa nchini; Chuo cha Ufundi Arusha, pamoja na Chuo cha Ufundi cha Dar es Salaam, (Dar es Salaam Institute of Technology) ambao sasa tayari wanaendelea kutengeneza mita hizi. Lengo ni kuona tunataka kusambaza mita kwa bei nafuu. Kwa sababu mita za awali tulikuwa tumezitoa nje, bei kidogo ilikuwa juu kwa wananchi, nasi kama Serikali tunaangalia uwezekano wa kumpunguzia gharama za maisha mlaji wa mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi la ufungaji mita za malipo kabla, zitaendelea vizuri na siyo tu kwa Arusha, bali nchi nzima. (Makofi)