Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdi Hija Mkasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:- Je, lini Kituo cha Polisi Micheweni kitakarabatiwa ili kiendane na hadhi ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. ABDI HIJA MKASHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni muda gani tangu Jeshi la Polisi lifanye tathmini ya ukarabati wa kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tathmini ilifanyika mwaka jana, 2023. Nami nimhakikishie Mheshimiwa Mkasha, kwa sababu, liko kwenye bajeti ya 2023/2024, mara fedha hizo ambazo tayari zimeombwa Hazina zitakapotoka, kituo hiki kitaanza kukarabatiwa. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:- Je, lini Kituo cha Polisi Micheweni kitakarabatiwa ili kiendane na hadhi ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Katika eneo la Somanga, Serikali iliahidi kwamba italeta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo Polisi chenye hadhi ya Wilaya. Eneo limeshapatikana, fedha kiasi cha shilingi milioni tatu za Mfuko wa Jimbo zimeshakwenda; je, ni lini Serikali italeta fedha hizo ili kituo hicho kiendelee kujengwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Ndulane kwa swali lake na kwa jitihada alizofanya hadi kuniita nikaenda kukagua eneo lile kwa ajili ya ujenzi wa Kituo hiki cha Polisi. Ni bahati mbaya eneo lililokuwa limetengwa mwanzo lilikuwa dogo, sasa kama wanatuhakikishia kwamba eneo limepatikana, then tutawaelekeza Maafisa wa Jeshi la Polisi wanaohusika na ujenzi, wakakague kwa madhumuni ya kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kituo hicho, nashukuru. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:- Je, lini Kituo cha Polisi Micheweni kitakarabatiwa ili kiendane na hadhi ya Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua Serikali ina mpango gani wa haraka kuzuia utekaji unaoendelea katika Jiji la Dar es Salaam na kupoteza maisha ya watu, kwa sababu, utekaji huu unaendelea kila kukicha? Nataka kujua, Serikali ina mpango gani wa haraka kuzuia jambo hilo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussien Amar, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunafuatilia kwa karibu matukio aliyoyaeleza kwamba yanaendelea kutokea katika Jiji la Dar es Salaam kwa madhumuni ya kudhibiti na kuwachukulia hatua za kisheria wale ambao wanahusika katika hicho kilichoitwa utekaji.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:- Je, lini Kituo cha Polisi Micheweni kitakarabatiwa ili kiendane na hadhi ya Wilaya?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi hii ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza sana Naibu Waziri, kaka yangu Mheshimiwa Sagini kwa kufuatilia kwa ukaribu sana harakati za ujenzi na ufunguzi wa Kituo cha Polisi Nanjirinji, alikwenda mwenyewe na ninashukuru sasa Kituo cha Polisi Nanjirinji kimeanza kazi. Pamoja na hayo, bado kuna changamoto za vitendea kazi ambavyo ndani yake ni too professional.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari sasa kutoa maelekezo kwa uongozi wa Polisi wa Mkoa wa Lindi ili waende wakazungumze na Maafisa au Askari pale Nanjirinji kwa lengo la kujua changamoto zao za kazi ili hatimaye usalama uendelee kuimarishwa pale Nanjilinji?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Ally Kassinge kwa namna alivyofuatilia kituo hicho hadi ikanilazimu Naibu Waziri kukitembelea kwa madhumuni ya kukianzisha. Changamoto ya ucheleweshaji wa kuanzisha tuliimaliza siku ile na baada ya wiki mbili kikaanza kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwahidi Mheshimiwa Mbunge, kwa vile tayari Serikali kupitia Jeshi la Polisi imesharidhia kituo kile kianze kutoa kazi, nitoe maelekezo kwa Mkuu wa Polisi nchini afuatilie kuona kwamba kituo kile kinapata vitendea kazi muhimu kuwezesha majukumu ya ulinzi wa raia na mali zao yaweze kufanyika kwa ufanisi, ahsante.