Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwa wananchi wanaoishi kwenye mitaa 17 ya Mamlaka ya Mji Mdogo Rulenge – Ngara?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa kuwa tayari Ngara kuna mkandarasi anayeendelea kujenge miundombinu ya kupeleka umeme maeneo ya Ngoma, Kata ya Bugarama, Kibogora, Mganza na Keza, na kwa kuwa mkandarasi huyu mpaka sasa hajapeleka umeme kwenye kata hizo na vijiji ambavyo viko viko kwenye kata hizo, ni upi mpango wa Serikali wa kumsukuma mkandarasi huyu ahakikishe anakamilisha kazi yake ya kupeleka umeme kwenye maeneo haya, ahsante. (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo ya Serikali, yako wazi kwa wakandarasi wanaoendelea na miradi ya kupeleka umeme vijijini kwamba wanapaswa kuheshimu mikataba yao. Wale ambao hawataweza kupeleka umeme kwa mujibu wa mikataba yao, basi wanakuwa wamejiweka kwenye mazingira ambayo hawatapata mikataba mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kuwakumbusha wakandarasi wote, wafanye kazi walizopewa kwa mujibu wa mikataba yao, maana kushindwa kufanya hivyo wanajihakikishia kwamba hawatapata mikataba mipya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, natoa maelekezo kwa watendaji wetu katika mkoa ule, wamsimamie kwa karibu mkandarasi huyu ili aweze kutimiza wajibu wake. (Makofi)