Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia Televisheni ya Taifa na Redio katika kutoa elimu ya kilimo salama na chenye tija?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninaomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na kilimo cha mbogamboga pembezoni mwa mito na mifereji inayotiririsha maji machafu kutoka viwandani katika majiji makubwa hasa Dar es Salaam.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa wananchi hawa ili waweze kukiuka athari ambazo zinaweza kutokea kiafya?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri amesema wanatoa elimu kwa njia ya nadharia na vitendo. Kwa Mkoa wa Dar es Salaam, kwa mwaka huu wametoa elimu mara ngapi na maeneo gani? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, ni kweli nikianza na swali la pili, takwimu kwa hapa siwezi kuwa nazo niwe mkweli nitalifanyia kazi.

NAIBU SPIKA: Jibu la kwanza.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hilo suala la pili, ni kwamba tutaendelea kutoa elimu. Vilevile, katika maeneo ambayo yana athari, kuna kanuni ziko katika ngazi za halmashauri ambazo zinapaswa kusimamiwa ili kuondoa kero hii ambayo Mheshimiwa Mbunge umeiainisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuhakikishie tu kwamba, sisi kama Wizara ya Kilimo tutaendelea kuelimisha wananchi wetu na vile vile tutazihamasisha halmashauri ziweze kutekeleza sheria na kanuni za halmashauri kwenye kusimamia yale maeneo ambayo yako katika mito na vile viwanda vinavyotiririsha majitaka katika maeneo ya wananchi, ahsante sana.