Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, Serikali imefanya utafiti kuhusu uwepo wa Madini Mkoani Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua baada ya utafiti huo wa awali kuna muendelezo gani katika ugunduzi huo wa madini?

Swali langu la pili, ni kwa kiasi gani wananchi wa Mkoa wa Mtwara wanafahamu maeneo hayo yenye madini ili waweze kuitumia fursa hiyo kujipatia kipato? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa hatua zinazochukuliwa baada ya madini kutambulika maeneo yenye madini hayo, Afisa Madini ya Mkoa anao wajibu wa kupeleka taarifa hizo kwa Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya, aidha kupitia machapisho ambayo GST wanaandaa. Mwaka huu mwezi wa Tano waliandaa kitabu cha madini yapatikanayo katika Wilaya zote za Tanzania, wananchi hufikishiwa taarifa pia kupitia mafunzo mbalimbali ambayo Wizara inatoa na kupitia utaratibu huo wananchi wengi wamejitokeza kwenda kukata leseni za utafiti na uchimbaji wa madini yaliyobainika katika hayo maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali lake la pili kwamba wanayafahamu maeneo hayo? Jibu ni ndiyo kwa sababu ya taarifa ambazo Wizara inasambaza kupitia GST na taasisi zingine za Wizara na ndiyo maana sasa hivi madini ya graphite yameanza kuchimbwa na wachimbaji wadogo ambao wamepata leseni na wanaendelea na utafiti.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha katika maeneo yenye dhahabu kama Nanyumbu na Masasi wachimbaji wadogo wameendelea kufaidika na Wizara sasa hivi iko katika mchakato wa kufanya utafiti wa kina zaidi ili wajue kiasi na aina ya madini na ubora wa madini yanayopatikana katika maeneo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)