Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini elimu ya uvuvi na mikopo ya vifaa vya kisasa vitatolewa kwa wananchi wa Manda, Ruhuhu, Iwela, Lupingu, Lifuma, Makonde, Kilondo na Lumbila?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na nimshukuru Mheshimiwa kwa majibu mazuri, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 Kata hizo Nane zina jumla ya wananchi 26,582. Je, kwa idadi hiyo ya boti mbili Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi kwamba Serikali inatakiwa iongeze boti?

Swali la pili, wavuvi wa Jimbo lile wana changamoto nyingi na wana maoni mengi ambayo wangetamani wakae na Mheshimiwa Waziri. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari kutangulizana na mimi baada ya Bunge hili kwenda kukaa na wavuvi wa Jimbo la Ludewa?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, zoezi la ugawaji wa boti lilianza kwa zoezi la awali Mheshimiwa Rais amekwishatoa maelekezo kwamba tuangalie maeneo yote yenye uhitaji wa kuongeza boti hizo na tayari tumeshaainisha maeneo ambayo yana umuhimu wa kuongeza boti na sasa Wizara iko tayari kuongeza boti kulingana na mahitaji ya maeneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kuhusu kuwatembelea, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Kamonga kwa jinsi ambavyo anafuatilia sana shida za wananchi wake na kuwatatulia, kwa kadri hiyo na sisi Wizara tuko tayari kufika katika eneo lake kwenda kuzungumza na wavuvi hao kuona namna sahihi ya kutatua changamoto wanazopitia wavuvi hao.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)