Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha zote za ujenzi wa barabara ya lami Karatu – Mbulu – Hydom hadi Sibiti ili ujenzi uendelee?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa sasa barabara hii ya Mbulu – Garbabi ni kweli Mkandarasi yupo site, lakini ana tatizo hilo la kutolipwa fedha baada ya yeye ku-raise certificate ambayo iko ofisini kwa Mheshimiwa Waziri. Je, lini atalipwa hiyo fedha ili aendelee kuweka au kumalizia barabara hii ya Garbabi kwenda Mbulu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, nashukuru kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri alikuwepo katika kusaini Mkataba wa Barabara ya kutoka Haydom kuja Labay. Sasa ni miezi sita, tumesaini tarehe 25 Mei, 2023. Je, ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili wananchi waweze kupita? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkandarasi ambaye anafanya kazi kati ya Mbulu na Garbabi, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba anaendelea na kazi kwa sasa. Hii ni baada ya Mkataba wake unamtaka asisimame kazi baada ya kuanza kazi. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, nimepata taarifa leo kwamba kazi zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipande alichokisema cha Labay – Haydom, ni kweli kilisainiwa. Nataka kumkumbusha Mheshimiwa Mbunge kwamba utaratibu unaotumika katika kipande hiki ni sanifu na jenga. Wajibu wa Mkandarasi kwanza ni kufanya usanifu wa ile Barabara. Halafu ikishasanifiwa ipate kibali kwamba iko sawasawa na Mamlaka kwa maana ya TANROADS ndipo anatakiwa sasa aanze kujenga hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hizo zinaendelea na akishakamilisha, basi tutamwona site akiwa anaanza kuijenga hiyo barabara, ahsante. (Makofi)

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha zote za ujenzi wa barabara ya lami Karatu – Mbulu – Hydom hadi Sibiti ili ujenzi uendelee?

Supplementary Question 2

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini Barabara ya Moshi – Arusha hasa kipande cha pale Moshi Mjini itapanuliwa ukilinganisha kwamba tayari Mikataba ilishasainiwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni kweli kwamba barabara hii inapanuliwa kutoka Arusha kwenda Moshi ikiwa ni pamoja ya lile Daraja la Kikafu. Hii barabara ambayo ameisema, tunasaidiana na wenzetu wa JICA. Ziko taratibu ambazo zikishakamilika, basi barabara hii itaanza kujengwa, lakini iko mbioni kuanza kujengwa. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha zote za ujenzi wa barabara ya lami Karatu – Mbulu – Hydom hadi Sibiti ili ujenzi uendelee?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Omurushaka kwenda mpaka Mrongo, Mkandarasi amepatikana ni zaidi ya miezi sita lakini bado Mkataba haujasainiwa. Je, ni lini Mkataba utasainiwa ili barabara hii ianze kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Moja ya swali ambalo alitolea ufafanuzi Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, ni kwamba Barabara aliyoitaja Omurushaka kwenda Murongo, kilometa 50 ni kati ya zile barabara kuu 15 ambazo tayari tumeshaomba kama alivyosema Mheshimiwa Waziri zisainiwe zote kwa pamoja ambazo zinagharimu karibu shilingi Trilioni 2.0. Alishasema kwamba aliomba Mamlaka ziweze kusimamia hilo zoezi, kushuhudia. Kwa hiyo namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo ni kati ya barabara hizo ambazo zitapata kibali cha kuanza kuzijenga, ahsante. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha zote za ujenzi wa barabara ya lami Karatu – Mbulu – Hydom hadi Sibiti ili ujenzi uendelee?

Supplementary Question 4

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa kuwa Mwezi Juni mwaka huu tulisaini Mkataba wa Barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Lalago. Je, ni lini kazi rasmi itaanza ya ujenzi wa kipande cha Karatu – Mbulu ambako kipindi hiki cha mvua wananchi wanapata matatizo makubwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipande cha Karatu – Mbulu ni kipande ambacho kinaangukia kwenye zile barabara ambazo zinajengwa kwa Mpango wa EPC+F. Tayari Wakandarasi washasaini, wako site wakiwa pia wanafanya, tunasema usanifu wa kina kwa sababu usanifu waliopewa ni wa awali. Baada ya kukamilisha taratibu zote kama tulivyosema, barabara hizi zitaanza kujengwa kuanzia Januari, ahsante.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha zote za ujenzi wa barabara ya lami Karatu – Mbulu – Hydom hadi Sibiti ili ujenzi uendelee?

Supplementary Question 5

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakamilisha Barabara inayoanzia Njuki – Ilongero – Haydom kwa kiwango cha lami hasa ukizingatia ujenzi wake umekuwa ukisuasua. Barabara hii ina ahadi ya viongozi toka Awamu ya Nne? Napenda kupata commitment ya Serikali, ni lini barabara hii itakamilika kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kama alivyosema ahadi za viongozi, namhakikisha Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara hizi zote ambazo zimepangiwa bajeti kwa mwaka huu, yako maandalizi ambayo yanaendelea kuhakikisha kwamba tunaanza ujenzi kama tulivyopanga kwenye Bajeti ya mwaka huu 2023/2024, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha zote za ujenzi wa barabara ya lami Karatu – Mbulu – Hydom hadi Sibiti ili ujenzi uendelee?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya kutoka Kalela – Munzeze – Buhigwe kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Genzabuke kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ni barabara ya mkoa ambayo namkumbusha Mheshimiwa Mbunge kwamba ilikuwa haijafanyiwa usanifu. Sasa hivi barabara hiyo inakamilishwa kufanya usanifu kutoka Kalela – Munzeze – Buhigwe. Baada ya hapo gharama zitajulikana, Serikali sasa itatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.