Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka utaratibu ili bei ya mafuta ya dizeli na petroli iwe moja kwa nchi nzima?

Supplementary Question 1

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, ukizingatia kwamba Bandari ya Dar es Salaam ni bandari ya nchi nzima siyo Dar es Salaam peke yake, lakini tumeona kwamba mafuta kwa maana ya petroli na dizeli zimekuwa rahisi zaidi Dar es Salaam kuliko maeneo mengine ya pembezoni. Kwa mfano, kwa Taarifa ya EWURA ya jana petroli Dar es Salaam ni 3,257 na dizeli 3,210 lakini ukienda Songwe ni 3,374 na dizeli ni 3,227 na maeneo mengine hali kadhalika.

Mheshimiwa Spika, maswali yangu mawili ya nyongeza; la kwanza; je, Serikali inategemea kumaliza lini tathmini hiyo ili utekelezaji huu uanze mara moja na wananchi walioko nje ya Dar es Salaam waepuke hiyo changamoto? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba inatatua changamoto za nyuma kama ambavyo imezisema kwenye majibu yake ya leo? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kumaliza tathmini yalikuwa ni maelekezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, kufanya tathmini hii kwa haraka sana ili kuweza kujua kama tunaenda kwa mfumo huo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge suala hili ni la kipaumbele na tathmini itakamilika hivi karibuni na kisha tutaweza kufanya tathmini, ili kuweza kujua kama kweli tunaweza kwenda kwenye mfumo huo. Kwa hiyo, ni suala la kipaumbele kwa upande wa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile tathmini itatueleza namna ambavyo tulipata changamoto huko nyuma na kwa sasa tujipange vipi ili kuelekea kuwa na mfumo huu kama tathmini itatuelekeza hivyo. Ahsante.