Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha usanifu wa mradi wa maji ya Mto Rufiji yatokayo Bwawa la Julius Nyerere kupeleka Mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, ningependa kupata commitment ya Serikali kwamba usanifu huu wa awali utakuwa umekamilika kufikia mwaka ujao wa fedha, ili tuweze kujua kwamba tatizo hili linaenda kutatuka kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Serikali haioni haja ya kwenye miradi yote ya uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji, sasa Wizara ya Maji iweze kubeba yale maji yanayotumika baada ya kuzalisha umeme na kwenda kusambaza kwenye maeneo ya jirani? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayofanya, lakini kubwa Wizara ya Maji mkakati wake mkubwa sasa hivi ni kuhakikisha kwamba tunatumia vyanzo toshelevu kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji. Moja ya mkakati ni kuhakikisha kwamba tunatumia maji haya ambayo yanazalishwa katika Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere. Pia tumeshaianza kazi ya kuyatoa maji ya Mto Ruvuma kuyapeleka katika Jimbo la Nanyumbu, lakini maji yale yatafika mpaka Jimbo la Masasi ili kuhakikisha wananchi wa Masasi wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la haja ya kuyachukua na kuyasambaza maji yanayotoka katika maeneo ya uzalishaji wa umeme, Serikali inaona haja hiyo, maji yale baada ya kupotea tutayatumia katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha watu wanapata huduma ya maji safi na salama.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha usanifu wa mradi wa maji ya Mto Rufiji yatokayo Bwawa la Julius Nyerere kupeleka Mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itafanya mradi wa kuvuna maji na kuboresha Mto Lumemo ili kupunguza adha ya mafuriko kwa wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, uikizingatia nchi yetu haina umaskini kwa maana ya mvua na mvua badala ya kuwa fursa imekuwa ikileta maafa mengi sana. Sasa maelekezo ya Mheshimiwa Rais kupitia Wizara yetu ya Maji na sekta zingine ni kuhakikisha kwamba, tunajenga mabwawa ya kimkakati na tumekwishaanza Bwawa la Kidunda na sasa hivi Bwawa la Farkwa, lakini pia tumepewa mitambo kwa ajili ya uchimbaji wa mabwawa. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kaka yangu Mheshimiwa Asenga, Ifakara tutaipa kipaumbele hasa juu ya mitambo tuliyokuwa nayo ili kuondokana na adha hii ya mafuriko kwa wananchi wa Ifakara.