Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaipatia Hospitali ya Wilaya ya Handeni Gari la kubebea Wagonjwa?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii niulize swali moja la nyongeza. Kutokana na ugumu wa jiografia za halmashauri, majirani zetu, hospitali hii imekuwa ikihudumia wagonjwa kutoka Mvomero, Chalinze, Kilindi, Handeni DC pamoja na kwetu Handeni Mjini.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutuongeza walau tuwe na ambulance mbili kwenye hospitali hii ili kuhudumia wagonjwa wa halmashauri hizi zinazotuzunguka? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Kwagilwa kwa kazi kubwa anayoifanya kuwasemea wananchi wa Jimbo la Handeni Mjini. Nimhakikishie tulifanya ziara pamoja kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Handeni, tuliona mahitaji yale na nimwahidi kwamba kwenye magari haya ambayo yatanunuliwa kwanza moja lazima apate lakini tutafanya tathmini kuona uwezekano wa kupata gari lingine kwa ajili ya Halmashauri yake. (Makofi)

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaipatia Hospitali ya Wilaya ya Handeni Gari la kubebea Wagonjwa?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kituo cha Afya cha Kinesi ambacho kinahudumu kama hospitali kwa maeneo ya Tarafa ya Suba ni kituo cha afya ambacho hakina gari kwa ajili ya kubebea wagonjwa. Sisi kama halmashauri tulikubaliana tutapeleka gari kupitia yale magari ya UVIKO ambayo Serikali ilituahidi kwamba yatakuja kwenye halmashauri ambazo zilitajwa. Nataka nijue sasa Serikali imefikia wapi kupata yale magari ili yaweze kwenda kwenye Kituo cha Afya cha Kinesi kwa ajili ya kutoa huduma kwenye maeneo yale? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jafari Chege, Mbunge wa Jimbo la Rorya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Serikali itapeleka magari ya wagonjwa kwenye halmashauri zote, lakini ni maamuzi ya halmashauri kuamua gari liende hospitali ya halmashauri au Kituo cha Afya ambacho wanaona ni kipaumbele zaidi katika halmashauri husika. Kwa hiyo, ni maamuzi yao katika halmashauri kwa kushirikiana na wataalam wa afya kufanya maamuzi hayo, lakini nimhakikishie kwamba mapema Julai au mwanzoni mwa mwezi wa Agosti, 2022, magari haya yatakuwa yamefika kwenye halmashauri zetu. Ahsante. (Makofi)