Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: - Je, kwa nini Baraza la kushauri masuala ya Watu Wenye Ulemavu linashindwa kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 1

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini kwa kuwa kumekuwepo na minong’ono ya kutokukaa kwa Baraza hili, sasa naomba Serikali iuambie umma wa Tanzania ni lini mara ya mwisho hili Baraza limekaa?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Baraza hili mbali na minong’ono ambayo inasikika lakini uhalisia wa Serikali ni kwamba, Baraza hili tayari lilikwishaundwa na Mheshimiwa Rais kwa mujibu wa kifungu cha 11 ambaye ndiye anakuwa na wajibu wa kumteua Mwenyekiti na Mwenyekiti wake ni Dkt. Kija Luhende na Katibu wake anakuwa ni Mkurugenzi wa masuala ya watu wenye ulemavu. Mara ya mwisho wamekaa katika kikao chao mwezi wa Disemba mwaka 2023.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo majukumu yanaendelea kutekelezwa na wajumbe wanakuwa 15 ambao wanateuliwa na Mheshimiwa Waziri na tayari wajumbe hao wapo na kazi zinaendelea kufanyika. Hivyo, kazi mojawapo ambayo waliifanya ni pamoja na kushauri kuhusiana na marekebisho ya sera ya watu wenye ulemeavu ambayo kwa sasa imedumu kwa kipindi cha muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, pia jukumu la pili, ni pamoja na kwenda kufanya maandalizi ya kuboresha Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010. Ahsante.