Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati shule kongwe za msingi zilizopo Mbarali ambazo zipo katika hali mbaya?

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza nitakuomba mwongozo wako kwenye swali hili kwa sababu hizo milioni 360 zilifika katika Shule za Chimala, Igalako, Lujewa na Isitu kujenga madarasa mapya na siyo ukarabati wa shule kongwe. Kwa hiyo baadhi ya madarasa haya 18 yalijengwa kwenye shule hizi. Ninachokitaka mimi kwa Serikali lini wataanza ukarabati wa shule kongwe Mbarali? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli, kama ambavyo Mheshimiwa Bahati Ndingo alivyosema kwamba swali lake la msingi ni ukarabati wa shule kongwe, lakini ukarabati unategemea na hali ya uchakavu wa madarasa, yapo madarasa ambayo yamechakaa kiasi cha kutokarabatika beyond repair. Sasa Serikali inachofanya ni kujenga madarasa mengine katika shule hizo na kuvunja madarasa ambayo tayari yamechakaa kiasi hicho.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hili ndiyo lililofanyika katika shule hizi ikiwa ni sehemu ya ukarabati, lakini hatulazimiki kukarabati madarasa ambayo yana miaka sitini, yameshachokahayakabaratiki tena itakuwa ni matumizi mabaya ya fedha za Serikali. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kukarabati, kama tulivyofanya hivi katika shule hizi kwa namna ya kujenga madarasa mapya au kwa namna ya kukarabati madarasa ambayo yapo katika hali ambayo yanaweza kukarabatika. Nakushukuru. (Makofi)