Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati shule chakavu za msingi katika Jimbo la Lushoto?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini kuna shule ambazo zina hali mbaya sana. Kwa mfano Shule ya Kwemashai, Shule ya Mshizii, Shule ya Msingi Kwai, Shule ya Msingi Matego, Kweboma pamoja na shule nyingine za Jimbo la Lushoto.

Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itapeleka fedha za dharura kwa ajili ya kukarabati shule hizo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na uchakavu wa shule lakini unaenda sambamba na ujenzi wa majengo na nyumba za Walimu. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za Walimu ili Walimu wetu hawa wasitembee umbali mrefu na vituo vyao vya kazi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge, amesema kwamba kuna baadhi ya shule ambazo zina uchakavu wa hali ya juu zaidi na kwa kweli zinahitaji bajeti maalum kwa ajili ya kuzikarabati. Kwa hiyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inatambua kwamba kuna shule ambazo zinahitaji maalum na tayari imeshaweka mkakati wa ukarabati wa shule hizo.

Mheshimiwa Spika, tumeanza na shule kongwe za sekondari baadhi ya shule zimekarabatiwa, bado nyingi zinahitaji ukarabati, lakini tuna shule nyingi za msingi ambazo tumeanza ukarabati na zoezi hili ni endelevu. Kwa hiyo naomba nitumie nafasi hii kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Lushoto kutuma wahandisi wa halmashauri hiyo ili kufanya tathmini ya mahitaji ya ukarabati kwa shule ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja na kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili fedha iweze kutafutwa, lakini pia kutafutwa mapato ya ndani kwa ajili ya ukarabati.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali imeweka mkakati wa ujenzi wa nyumba za Walimu. Tumeanza kujenga nyumba za three in one, two in one lakini na zoezi hili linaendelea kila bajeti ya kila mwaka, tutahakikisha tunajenga nyumba za Walimu katika shule zetu. Ahsante. (Makofi)

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati shule chakavu za msingi katika Jimbo la Lushoto?

Supplementary Question 2

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Je, ni lini Serikali itakarabati Shule chakavu za Msingi katika Jimbo la Busanda ikiwemo Lubanda, Lulama na nyinginezo nyingi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunatambua katika Jimbo la Busanda pia kuna shule chakavu. Tayari Serikali imeshaanza kuwaainisha shule chakavu zaidi katika majimbo yote kote nchini na fedha zinatafutwa kwa ajili ya kuanza ukarabati kwa awamu. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Jimbo la Busanda pia litapewa kipaumbele. Ahsante.