Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kupandisha madaraja kwa mserereko Walimu wenye changamoto ya kupandishwa madaraja wakiwemo wa Ngara?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nashukuru, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa kuna Walimu waliajiriwa 2013 na kumekuwa na upandishwaji wa madaraja kwa makundi huku Walimu walio wengi wakiachwa nyuma bila kupandishwa madaraja kutoka 2013. Ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha Walimu hawa wanapandishwa madaraja?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa kuna kundi kubwa sana la Walimu wa Jimbo la Ngara ambao ni Walimu wa grade A ambao walitakiwa kuwa wamepandishwa mpaka kuwa grade G mpaka sasa hivi lakini wengi wameachwa nyuma na michakato hiyo. Ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha Walimu hawa wanapandishwa madaraja? Ahsante. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika majibu ya msingi, kwa kuwa vipo vigezo vinavyotumika kwa ajili ya kupandisha madaraja Walimu, nataka kulihakikishia Bunge lako kwamba ule uchambuzi wa uhakiki uliokuwa unafanyika umekwishakamilika kwa upande mmoja ambapo katika Mwaka huu wa Fedha unaokwisha 2023/2024, Serikali inatarajia kupandisha Walimu 52,551 wakiwemo Walimu 148 wa Halmashauri ya Ngara ambao wamekwishatimiza vigezo vinavyotakiwa. Nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako kwamba, Walimu hawa tutawapandisha.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la Walimu ambao wamepandishwa katika grade nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Halmashauri ya Ngara kwamba, Serikali ilifanya uhakiki na uchambuzi wa walimu 283,193 wa halmashauri zote nchini. Katika uchambuzi huo tulibaini kwamba Walimu 54,242 wamekwishatimiza vigezo kwa wale ambao wanapandishwa madaraja na kati ya hao Walimu 540 wakiwemo wa Halmashauri ya Ngara na Halmashauri nyingine za Mkoa wa Kagera, ambao walikumbwa na changamoto hizo wamethibitika kwamba wamepata vigezo hivyo, wote kwa pamoja nao tutaweka katika mserereko ili waweze kufika katika madaraja wanayotakiwa.