Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara hii imesainiwa tarehe 19, ni zaidi ya mwezi mzima tangu imesainiwa. Je, ni lini mkandarasi atakabidhiwa site ili aanze kazi rasmi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Barabara ya Omugakorongo – Kigarama mpaka Mrongo ilitangazwa kujengwa kwa kiwango cha lami, lakini mpaka sasa hivi haijulikani ni hatua gani imefikia ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kyerwa kwamba, baada ya kusaini barabara hii kinachofuata sasa ni kumkabidhi mkandarasi ili aanze kazi. Tayari Meneja wa Mkoa wa Kagera ameshapewa maelekezo na TANROADS Makao Makuu kwamba kuanzia tarehe 5 mwezi huu, siku yoyote huyu mkandarasi aweze kukabidhiwa kazi na aanze kazi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la Barabara ya Omugakorongo – Murongo, ilikuwa tayari imeshapata mkandarasi, lakini kwa taratibu za kimkataba, yuko mkandarasi ambaye ali-appeal, yaani alipinga mchakato wa manunuzi na hivyo imeamuliwa kazi hiyo itangazwe tena. Kwa hiyo, tuko kwenye hatua nyingine ya manunuzi baada ya ule mkataba wa kwanza kuonekana kwamba ulikuwa na changamoto za kisheria. Kwa hiyo, taratibu zinaendelea, tayari tuko kwenye manunuzi tena. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Barabara ya Masasi mpaka Liwale, kilometa 175, ni barabara ambayo imesainiwa tarehe 16 mwezi wa Sita mwaka uliopita 2023 kuwa itajengwa kwa EPC+F, lakini barabara hii usanifu wake …

SPIKA: Mheshimiwa Kuchauka, uliza swali. Umeshaona wenzio wengi wamesimama hapa na tuna dakika chache tu. Hizo taarifa nyingine zote Waziri anazijua, wewe nenda kwenye barabara yako.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, wana-Liwale wamenituma niulize, barabara hii ujenzi wake unaanza lini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara aliyoitaja itaanza kujengwa mwaka huu kama tulivyokuwa tumeahidi. Ahsante.

SPIKA: Mwaka huu ukimaanisha 2023/2024 au 2024/2025?

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, tunategemea kuanza ujenzi wa barabara hiyo mwaka huu wa fedha.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Mkataba wa Ujenzi wa Barabara ya Ruaha National Park utasainiwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, Barabara ya Iringa – Msembe – Ruaha National Park, sasa hivi tuko kwenye evaluation na inafadhiliwa na World Bank. Baada ya kukamilisha taratibu hizo, barabara hiyo itaanza kujengwa. Ahsante.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, Serikali ina kauli gani kwa barabara ya Iringa (MR) – Pawaga Road (Itunundu) ambayo mkandarasi ametelekeza vitu na haendelei na wakati alikuwa ameichimbachimba, hivyo wananchi kupata shida?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge, baada ya hapa tuweze kukutana naye ili niweze kujua changamoto ya huyo mkandarasi na tuweze kuondoa hiyo changamoto ambayo mkandarasi anaileta kwa wananchi. Ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 5

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, je, ni lini Barabara ya bypass inayoanzia Kata ya Kisaki mpaka Mtipa itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara hii ilishasanifiwa na Serikali kwa kweli inaendelea kutafuta fedha ili kuweza kuijenga hiyo Barabara ya Bypass katika Mji wa Singida.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 6

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, ni lini ujenzi wa Barabara ya Mbagala Rangi Tatu mpaka Kongowe ambayo ipo katika bajeti ya mwaka huu utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara hiyo kilometa 3.8 imeshapata kibali cha kutangazwa ili ianze kujengwa. Ahsante.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 7

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, Barabara ya Kongwa – Kiteto – Simanjiro ni lini itaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, hiyo ni barabara ambayo iko kwenye EPC+F. Kama nilivyosema, tunategemea hizo barabara zianze kujengwa mwaka huu wa fedha. Ahsante.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 8

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, naomba kufahamu, je, Serikali imefikia hatua gani kwenye maandalizi ya kujenga barabara ya Hydom – Mogitu kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara hii ilishafanyiwa usanifu na tayari Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 9

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, ni lini Barabara ya Iguguno – Nduguti, Wilaya ya Mkalama itaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara hiyo itaanza kujengwa mwaka huu, lakini imeshapata kibali cha kuitangaza. Kwa hiyo, bado tunatangaza, lakini tuko kwenye hatua ya kuitangaza mwaka huu. Ahsante.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 10

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru, ni lini barabara ya Utegi – Shirati – Kilongwe itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara hii ndiyo kati ya zile barabara za kilometa 27 ambazo zimepewa kibali itangazwe kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Supplementary Question 11

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, ni lini Barabara ya Kongwa – Mpwapwa itaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, tayari mkandarasi alishapatikana, kwa hiyo, kinachosubiriwa sasa hivi ni kumkabidhi site. Ahsante.