Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO aliuliza:- Je, lini Bima ya Afya kwa watu wote itaanza kutumika?

Supplementary Question 1

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwanza naipongeza Serikali kwa majibu yake mazuri. Napenda kujua, katika utekelezaji wa Bima ya Afya, nini mkakati wa Serikali wa kuwasaidia akinamama wajane ambao hawatakuwa na uwezo wa kulipa Bima ya Afya? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; maeneo ya miji mikubwa kama Mkoa wa Mwanza kuna wimbi kubwa la watoto yatima na watoto wa mitaani. Nini mkakati wa Serikali wa kuwasaidia watoto hao kuweza kupata Bima ya Afya ili waweze kupata tiba bora?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa maswali yake mazuri. Moja, anazungumzia kwamba ni nini Serikali itafanya kwa akinamama wajane ambao hawana uwezo, kwa sababu inategemeana, kuna mjane, lakini ana uwezo na kuna wale ambao hawana uwezo. Ninyi Wabunge mnakumbuka hapa mlisisitiza utaratibu wa kuwasaidia wasio na uwezo na utaratibu huo huo utatumika kulisaidia hilo kundi ambalo amelitaja.

Mheshimiwa Spika, pia, amezungumzia watoto wa mtaani, nao vile vile wanaangukia kwenye eneo lile lile, lakini wote kwa pamoja suala la watoto wa mtaani tusione kama ni kundi maalum, tuone ni kundi la sisi kuhamasishana kuliondoa mtaani na kuhakikisha liko nyumbani, liwe na utaratibu mzuri. (Makofi)