Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, nini maandalizi ya Serikali kuhusu teknolojia ya kutengeneza watu wenye akili bandia na kulinda maadili ya Kitanzania?

Supplementary Question 1

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kuniruhusu niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, napenda kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza; matumizi ya artificial intelligence kwa maana ya ufahamu bandia (akili mnemba), tayari yameshaanza kutumika hapa nchini kwetu. Tarehe 27 Januari yalifanyika majaribio ya mwalimu kufundisha akiwa Kibaha akafundisha Shule ya Dodoma na limefanyika jaribio lingine la daktari akiwa Dar es Salaam akafanya upasuaji Zanzibar na ukafanikiwa.

Je, hatuoni sasa kwamba introduction ya artificial intelligence inawaondolea watu ajira zao kabisa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; matumizi ya roboti yanalenga kutatua tatizo la upungufu wa watu duniani. Nchi za Magharibi duniani ambapo roboti inatokea watu ni wachache, huku kwetu bado tupo na watu wengi sana. Itakuwaje tutakapofika wakati, mwalimu roboti, daktari roboti na rubani roboti; tutawapeleka wapi watu ambao tunawa-train leo.

Je, Serikali imejiandaa kujua cha kufanya baada ya roboti kuwa zimechukua ukanda wa ajira zote? (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na kumpongeza Naibu Waziri na Wizara ya Elimu kwa majibu mazuri na maandalizi mazuri, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mathias Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maendeleo ya sayansi na teknolojia na ubunifu duniani yametupitisha kwenye mapinduzi kadhaa ndiyo maana tuna mapinduzi ya kwanza ya viwanda, mapinduzi ya pili, mapinduzi ya tatu na sasa tupo mapinduzi ya nne na kuna nchi zimeanza mapinduzi ya tano na ya sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mapinduzi yaliyotokea yamekuwa na sifa zake na katika hizo sifa kumekuwa na faida na hasara ya kila mapinduzi kutoka mapinduzi mamoja kwenda mapinduzi mengine. Yapo ambayo yameleta faida, lakini pia yameleta hasara. Tukianza mapinduzi ya kwanza kuna watu walipoteza kazi na kuna watu walipata kazi; mapinduzi ya pili, kuna watu hivyo hivyo walipoteza kazi na kuna watu walipata kazi. Tunafaidikaje au tunapataje hasara inategemea na namna tulivyojipanga na kujiandaa kwa mapinduzi hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa haya mapinduzi ya nne yanajulikana, namna mnavyojiandaa, mnajiandaa kwa kuwa na mifumo mizuri ya sheria kwa maana ya legal framework, kuwa na sera, sheria na kanuni ambazo zitasaidia kuwalinda watu wenu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, mnakuwa na taasisi zitakazosimamia hayo mapinduzi na ya tatu, mnakuwa na uwekezaji kwenye hayo mapinduzi ili mtoke salama. Sasa Serikali imejipangaje? Kwanza, tumpongeze Rais Samia kwa maono yake ya kuanzisha Wizara inayoshughulikia TEHAMA, kwa sababu alipoingia madarakani akaianzisha Wizara. Kazi ya Wizara ni kuziandaa hizo sheria, kuandaa hizo taratibu, lakini pia kuziandaa taasisi na uwekezaji ili Taifa letu lipate faida katika matumizi ya akili bandia badala ya kupata hasara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilihakikishie Bunge lako na Bunge lina wajibu wa kuhakikisha sheria zinatungwa, taratibu zinawekwa ili wale watakaopoteza ajira kuwe na namna ambayo watashughulikiwa. Pia, tuliandae Taifa letu kwamba haya mabadiliko yana fursa ndani yake na ndiyo maana tunawafundisha watoto wetu, tunaandaa vyuo, tunaelimisha jamii ili tusipitwe kwa sababu haya mapinduzi hayakwepeki, lazima tujiandae kwenda huko mbele. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, nini maandalizi ya Serikali kuhusu teknolojia ya kutengeneza watu wenye akili bandia na kulinda maadili ya Kitanzania?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, kwanza kabisa nampongeza sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa katika teknolojia. Pia, kwa Serikali kutambua kwamba zipo faida za kutumia akili mnemba kwa maana ya artificial intelligence, lakini zipo athari kubwa hasa tukiangalia kwenye maeneo ya uchaguzi, hata kwenye maeneo ya elimu ambapo wanafunzi wanaweza wakatumia akili mnemba kuandaa research zao.

Sasa je, Waziri mwenye dhamana ya masuala ya teknolojia kwa maana ya akili mnemba (artificial intelligence) yupo tayari kutumia mamlaka yake ya kutumia kanuni kuona ni namna gani ambavyo sheria zitalinda Watanzania dhidi ya matumizi hasi ya artificial intelligence? (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Lugangira, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, suala la faida na hasara la artificial intelligence haliwezi kushughulikiwa kwa sheria moja na ndiyo maana hata wakati wa mjadala wa Sheria ya Uchaguzi tulisema hebu tupeni muda tutengeneze kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutatumia sheria zaidi ya moja kulishughulikia na juzi tumefanya mabadiliko hapa ya Sheria ya Miamala ya Kielektroniki na mengine, lakini bado kama Serikali tuko tayari na mimi kama Waziri nipo tayari kutumia mamlaka ya kisheria kutengeneza kanuni wakati tukisubiri hayo mabadiliko makubwa. Tutengeneze kanuni ili jamii yetu iendelee salama pia ifaidike na matumizi ya akili bandia. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, nini maandalizi ya Serikali kuhusu teknolojia ya kutengeneza watu wenye akili bandia na kulinda maadili ya Kitanzania?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na kwamba matumizi ya artificial intelligence yana faida na hasara kiuchumi, kijamii na kisiasa; nitaenda kuzungumzia zaidi madhara kwa mfano, katika kuingilia faragha za watu, uchumi…

MWENYEKITI: Naomba uulize swali la nyongeza.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua Serikali imejipangaje maana yake majibu ya Naibu Waziri hapa ameelekeza zaidi kwenye kuwekeza kujenga chuo, kufanya tafiti; Serikali mmejipangaje kimkakati kupeleka wataalam mbalimbali mathalani wa mahakamani, polisi na idara nyingine nyeti kuweza kuja kukabiliana na madhara hasi ya artificial intelligence?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kwa maana ya kulinda privacy za watu mtakumbuka Bunge hili limetunga Sheria ya Data Protection, sheria imesainiwa na Rais, kanuni zimekamilika na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imeshaundwa na imeanza kazi. Kwa hiyo, huko tuko salama lakini kwa maana ya training, mwaka huu wa fedha Wizara yangu ina-train watu 500 kwa wakati mmoja na hawa ni watumishi wa Serikali ili waende kukabiliana na haya mapinduzi ya viwanda yanayoendelea, tunawa-train ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile wakati huo katika majibu ya msingi tumeeleza kwamba kwa sababu training hizi ukiwa unapeleka nje peke yake ni ghali, tunaanzisha chuo cha kwetu wenyewe, kinajengwa Dodoma hapa Nala na kuna chuo kingine kinajengwa Kigoma na tuna centers nane tunazitawanya nchi nzima kwa ajili ya kutoa mafunzo ya kuwawezesha watu wetu wakabiliane na changamoto za akili bandia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wito wangu ni kwamba tusifikirie mabaya na changamoto peke yake kwenye matumizi ya akili bandia, badala yake tuangalie faida zitakazopatikana na akili bandia kwa maendeleo ya jamii yetu na kwa maendeleo ya uchumi wa nchi yetu. (Makofi)