Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ameir Abdalla Ameir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. AMEIR ABDALLAH AMEIR aliuliza:- Je, tafiti zipi ambazo Taasisi za Tiba Asili zimekamilisha na kuweza kuwa suluhisho la maradhi mbalimbali kama Tiba Mbadala?

Supplementary Question 1

MHE. AMEIR ABDALLAH AMEIR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa asilimia 60 ya Watanzania wanatumia matumizi ya tiba asili lakini kuna miti dawa isiyopungua 12,000. Swali langu liko hapa, je, ni miti gani maarufu ambayo inatumika ambayo tunayo hapa nchini katika kutengeneza tiba asili au kutengeneza dawa za kisasa katika hizo tafiti 50 ambazo Mheshimiwa Waziri umezieleza?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa mitidawa mingi ya asili inatoweka, ikiwemo miti dawa maarufu ikiwemo ule mti unaitwa BLUNAS AFRICANA ambao unatumika kutibia tezi dume, je, Mheshimiwa Waziri Serikali ina mkakati gani sasa wa kuinusuru hii miti ya asili inayopotea na iliyopotea na hii mingine ambayo iko hatarini kupotea? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia eneo hili nyeti na nimwambie tu kuna dawa, kuna miti ambayo iko Tanzania na inaoteshwa Tanzania na inatumika kutengeneza dawa ya Malaria kama hii yaluu ambayo tunayo tunaitumia kawaida hapa lakini kuna Mkunyinyi ambao uko kule kwa Mheshimiwa Shangazi ambayo nayo inatumika kutengeneza hii drip ya quinine, ipo mingi kwa sababu umesema 1000 na zaidi kwa hiyo ni shida kutaja yote hapa na kuna namna mbalimbali za kutengeneza dawa za binadamu.

Mheshimiwa Spika, suala lake la pili ni kuhusu kutunza hii miti maana yake mingi ipo Tabora, iko maeneo mbalimbali kwa kweli ni suala nyeti tunalichukua na tunashirikiana mpaka sasa na Wizara ya Maliasili kuhakikisha haya mambo muhimu kwenye nchi yetu yanatunzwa, na nikuombe na wewe na niombe Wabunge na Watanzania tutunze hii miti na tutunze mazingira kwa sababu tutafanya reservation ya hivi vitu muhimu kwenye nchi yetu na kwenye Wizara ya Elimu tutashirikiana nao ili kuweza kutengeneza watu wengi zaidi wenye akili vumbuzi kwa sababu sasa hivi tunatengeneza watu wengi wenye akili za kufanya kazi badala ya kutafakari. (Makofi)